MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 20 January 2015

BODI MPYA YA TANESCO CHINI YA WAZIRI MUHONGO HII HAPA

Wajumbe wa Bodi ya TANESCO wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Dkt. Mighanda J. Manyahi (wa sita kutoka kushoto) wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eng.Ngosi Mwihava (wa tano kulia) mara baada ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikati) kuizindua Bodi hiyo jijini Dar es Salaam.Wajumbe wengine wa Bodi hiyo (kutoka kushoto) ni Dkt. Nyamajeje C. Weggoro, Eng. Boniface C. Muhegi, Dkt. Mutesigwa I. Maingu, Bw. Shaaban S. Kayungilo, na Dkt. Haji H. Semboja. Wajumbe wengine (kutoka kulia) ni Bibi. Kissa Vivian Kilindu, Bw. Felix G. Kibodya na Eng. Juma F. Mkobya.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwapongeza Wajumbe wa Bodi mpya ya TANESCO mara baada ya kuizindua Bodi hiyo jijini Dar es Salaam na kutoa vipaumbele vya utekelezaji wa majukumu. Wanaoshuhudia ni viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini wakiongozwa na Naibu Waziri, Stephen Masele (kushoto kwa Waziri) na Kaimu Katibu Mkuu, Eng. Ngosi Mwihava (wa nne kulia).
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, Dkt. Mighanda J. Manyahi (aliyesimama) akizungumza mara baada ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuizindua Bodi hiyo jijini Dar es Salaam. Wanaomsikiliza ni Waziri, Profesa Muhongo (kulia) na Mjumbe wa Bodi hiyo, Dkt. Haji H. Semboja (kushoto).
Na Mwanaharakati.

No comments: