MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 6 January 2015

MAAJABU!!! ATAPIKA MFUPA WA SAMAKI BAADA YA KUISHI NAO KWA MIAKA MITANO.


Ni binti wa darasa la 7 Antia Hildephonce mwenye umriwa miaka 13, aliyekabwa na mfupa wa samaki akiwa darasa la tatu shule ya msingi Kibeta Bukoba mjini, ambapo inadaiwa wakati wote alikuwa akisikia maumivu kwa msimu.

Ametapika mfupa huo pichani pamoja na vipande vya minofu isiyoeleweka ni ya nyama gani pamoja na uchafu mwingine, huku akisema kabla ya kutapika alivimba tezi kwa muda wa siku tatu huku homa kali ikimshika na baada ya kutapika sasa anajisikia vizuri.

Ameuambia mtandao huu kuwa, alitunza siri ya maumivu yake kwasababu aliwahi kumweleza mama yake Winifrida       Mlama, kuwa alikabwa na mfupaa na wakati huo, ndipo mama yake akamkaripia na kutishia kumchapa hivyo akaogopa kusema hata wakati maumivu yalivyokuwa yakimsumbua anaamua kunyamaza.
Na Mwanaharakati.

No comments: