MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 12 January 2015

MGOMO WA WAFANYABIASHARA WA NYAMA BUKOBA KIZUNGUMKUTI, SOMAHAPA

 



Wakizungumza katika machinjio ya bukoba ambapo kwa siku ya leo wamesema kuwa hawawezi kuchinja nyama yoyote mpaka wafikie muafaka na serikali wamesema kuwa majibu yanayotoka katika mamlaka husika hayaridhisha katika upandishaji wa nyama.

Bwana RASHID ISMAIL, HAKIMU HUSSEIN  pamoja na EDWINI PASTORI wamesema kuwa kukosekana kwa ngombe katika mkoa wa kagera kunatokana na ngombe hao kuwa na soko kubwa katika baadhi ya nchi kama COMORO,SUDAN UGANDA pamoja na nchi nyingine.



Aidha wamesema kuwa  kupanda kwa kitoweo hicho kunasababishwa na mambo mengi ikiwemo kupandishiwa bei ya leseni pamoja na mambo mengine na kuiomba serikali kitafarkari suala hilo kwa makini.

Kwa uapnde wake mwenyekiti wa wachinjaji manispa ya bukoba bwana HATWIBU MUSA  amesema kuwa  sababu zinazotolewa na serikali hazina mashiko kutokana na kiwango kikubwa cha utoroshaji ngombe kwenda nje ya nchi.
Aidha ameongeza kuwa usimamaji wa uchinjaji wa ngombe hautaendelea mpaka pale wanatakapofikia muafaka kwani barua waliyoipokea jana inasema washushe kitoweo bila ya hivyo wasifungue bucha zao.

Bwana MUSA ameongeza kuwa awali walikaa na mkuu wa mkoa ambapo walikubaliana kupandishwa kitoweo hicho  lakini baadae makubaliano hayo yamekiukwa.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: