MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 7 January 2015

NEWS ALERT!!! TAARIFA KAMILI MBUNGE ATANGAZA KULIACHA JIMBO KAGERA




Akizungumza na mwananchi nyumbani kwake katika mamlaka ya mji wa Rulenge mbunge huyo amesema kuwa hahitaji kuendelea kuwa mbunge kwani umri wake nni wa kupumzika wananchi waridhike na yale aliyoweza kwa kipindi chake.

Amesema wakati akiingia madarakani kuongoza jimbo hilo aliahidi wananchi wa Ngara kupata nishati ya umeme hadi vijijini na juhudi zinaendelea baada ya umeme huo kuwashwa kupitia mpango wa usambazaji umeme vijijini (REA).

Amedai katika  tarafa ya kanazi, Nyamiaga, Murusagamba na Rulenge baadhi ya vijiji vimepata huduma ya maji kupitia mpango wa benki ya dunia na wananchi wamepinguza umbali wa kutafuta huduma hiyo umbali mrefu.

“Ofisi za serikali na mashirika nimewasumbua sana wakiwemo mawaziri kuwaomba wasaidie jimbo langu kuliwekea miundombinu ili wananchi wapambane kupunguza umaskini”. Alisema Ntukamazina.

Alisema changamoto  kubwa katika jimbo hilo ni hisia za ubaguzi wa kijiografia kuliingiza katika siasa kati ya jamii ya wahangaza na washubi  walioko katika kanda za Bugufi ngara kaskazini na Bushubi jimbo la Ngara kusini.

Alisema utofauti huo unachangia wananchi kutokuwa naumoja wa dhati katika kuleta maendeleo na kusababisha kukosa mtu makini wa kuweza kugombea nafasi ya ubunge kwa mwaka 2015.

Katika hatua nyingine amewaomba wananchi kupitia vikundi mbalimbali vya kijamii kumpata mrithi wake atakaye endeleza harakati za maendeleo na asiyetengeneza makundi ya kisiasa kidini ama kikabila wala kwa kuangalia rika.

Ntukamazina kabla ya kuwa mbunge alikuwa katibu mkuu utumishi kati ya mwaka 1991-1993 na amewahi kuwa msimamizi  wa uboreshaji utendaji kazi na kustaafu akiwa na umri wa miaka 55 ya kuzaliwa.

Awali katika utumishi wake  akiwa na fani ya ualimu amewahi kuwa  Makamu mkuu wa chuo cha Uongozi na maendeleo (IDM) Mzumbe 1978-1980.

Mwaka huo aliteuliwa na Rais Mwinyi kuwa mkurugenzi wizara ya mipango na wizara ya viwanda na biashara 1980 -1986 kabla ya  kuwa katibu mtendaji wa mashirika ya umma 425 na kuteuliwa kuwa katibu mkuu utumishi.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: