MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 24 February 2015

BREAKING NEWS!!! MAPIGANO MAKALI KATI YA POLISI NA RAIA, GARI YA POLISI YACHOMWA MOTO



Taarifa zinasema kuwa, mji mdogo wa Ilula, ulioko katika mkoa wa Iringa, umekumbwa na sintofahamu kubwa kufuatia mapigano baina ya Askari Polisi na raia.

Barabara zimefungwa na kusababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa barabara hiyo, huku ikielezwa kuwa gari la askari aina ya Hyundai, limechomwa moto na raia hao, ikisemwa kuwa polisi wamezidiwa.....


Inaelezwa kuwa, asubuhi ya leo, askari walifika katika eneo hilo kwa minajili ya kukamata watu waliokuwa katika vilabu wakinywa pombe muda huo wa kazi, ambapo katika kimbia kimbia ya wananchi kuwaepuka askari hao, mama mmoja alianguka ghafla na kupoteza maisha.

Chanzo chetu kinaendelea kutanabaisha kuwa, mama huyo alikuwa hajaguswa na askari hao, lakini wananchi ghafla wakaanzisha fujo wakidai kuwa kifo cha mama huyo kimetokana na askari hao na ndipo tafrani baina ya pande hizo mbili likazuka.

Hadi taarifa hizi zinawekwa hewani, inaelezwa kuwa askari walishazidiwa na kuwa walishaomba msaada wa Askari wa Kikosi cha Kuzuia Fujo (FFU), toka Iringa mjini, ambao walikuwa njiani kuelekea eneo la tukio.
Taarifa zaidi kuhusu tukio hili zitawajieni, pindi mawasiliano na mamlaka yatakapokamilika
 

Na Mwanaharakati.

No comments: