MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 26 February 2015

JINSI DADA WA AFANDE SELE ALIVYOFIA GEST, SOMA UNDANI WAKE

Dada wa msanii mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, 
Seleman Msindi Afande Sele Zaria Kambi (30) ambaye alikuwa ni mhudumu 
wa baa, amekutwa ameuawa kikatili katika Gesti ya Stavi (Gesti ya 
Marafiki) iliyopo Kichangani, mjini Morogoro.
 
Tukio hilo la kinyama lilitokea usiku wa Jumapili iliyopita baada ya 
marehemu kuwa amekubaliana kulala pamoja na mteja aliyekuwa akimhudumia 
kinywaji, ambaye pia alikuwa amechukua chumba katika nyumba hiyo hiyo 
iliyokuwa na baa.
 
Kwa mujibu wa rafiki wa marehemu, ambaye pia alikuwa ni mhudumu wa 
gesti hiyo, Rehema Saleh, alisema mtu mmoja asiyefahamika, alifika 
kazini kwao na kupanga chumba namba 8A na baadaye alienda upande wa baa 
kunywa pombe akihudumiwa na Zaria.
 
Mimi na Zaria (pichani) tunaishi jirani, sasa baada ya kumhudumia na
 yeye kununuliwa pombe, wakakubaliana walale pamoja, tunaishi jirani 
hivyo kila siku baa ikifungwa tunaongozana na jana tuliongozana njiani 
aliniambia amepata kichwa hivyo anakwenda nyumbani kuaga na baadaye 
arejee kwa bwanake huyo ambaye ni mara ya kwanza anaonana naye, 
alisema Rehema na kuongeza.
 
Cha ajabu saa 8 usiku napigiwa simu na mlinzi akidai Zaria 
amenyongwa na mteja wake, sikuwa na jinsi, kulipokucha nilifika hapa 
gesti na kukuta mwili wa marehemu ukiwa kitandani, alisema na kuangua 
kilio



Mlinzi wa gesti hiyo, John Emmanuel akizungumzia tukio hilo, alisema 
majira ya saa 6 usiku Zaria aliingia katika chumba namba 8A na saa moja 
baadaye, akasikia kelele zikitoka chumbani humo, ambazo alihisi ni za 
kimapenzi
 
Sijakaa vizuri saa 8 usiku jamaa alitoka na begi lake akitaka 
nimfungulie aondoke huku mkononi akiwa na tiketi ya basi kuelekea Mbeya,
 nikamwambia kwanza twende chumbani kwake nikachunguze ndipo nimruhusu 
atoke, awali aligoma na mimi nikagoma kumfungulia geti, tukaganda kama 
dakika mbili akakubali kwenda chumbani tulipofika tukamkuta Zaria 
amekufa huku akiwa mtupu, nikamjulisha bosi Pascal Mafikiri ambaye 
aliita polisi wakamchukua mtuhumiwa na mwili wa Zaria, alisema.
 
Mama mzazi wa marehemu, Mwajuma Hassani Kambi ambaye ni Mjumbe wa 
Serikali ya Mtaa wa Mwande Kata ya Kichangani kwa tiketi ya Chadema 
alipokea taarifa za kifo cha mwanaye Jumapili usiku
 
Alisema mwanaye ameacha mtoto anayeitwa Rashid lsmail Kaliembe ambaye
 anasumbuliwa na uvimbe tumboni na kwamba kila mwezi alikuwa akipelekwa 
Muhimbili kwa matibabu.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alithibitisha 
kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa, Erick Bruno, ambaye ni mkazi
 wa Manzese Tip Top Dar es Salaam, anashikiliwa. Marehemu huyo alizikwa 
Jumanne iliyopita mjini Morogoro.

Na Mwanaharakati.

No comments: