MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 21 March 2015

KAGASHEKI; WATENDAJI WA SERIKALI WASIHARIBU KAZI ZA WANANCHI KWA KUSINGIZIA WANASIASA KUWA NDIYO WANASABABISHA MATATIZO, AZUNGUMZIA MASUALA MATATU MAZITO MANISPAA YA BUKOBA.

UJENZI WA SOKO, MAUAJI NA UCHOMAJI MAKANISA PAMOJA NA USAJIRI WA PIKIPIKI


Balozi Kagasheki ambaye pia ni mbunge jimbo la Bukoba mjini CCM, amesema kuwa lazima masuala ya wananchi yasimamiwe kwa pamoja kwasababu wanasiasa wanafuta dola na kuajiri watalaamu watekeleze mambo ya wananchi.
Amesema kuwa kujenga soko la kisasa ni muhimu lakini wanatafuta sehemu pembezoni mwa mji ili kuupanua na watu wafanye biashara kwa uhuru, uhalifu ulioibuka manispaa ya Bukoba amesema kuwa wanashirikiana na kamanda wa polisi kuukomesha wanameshaweka mkakati mbadala lakini baadhi ya wavunjifu wa amani wasitumie siasa kuhatarisha amani iliyopo...................




Kuhusu kubadilisha namba za pikipiki kupitia TRA, Balozi Kagasheki amesema ni utaratibu muhimu wa serikali ambao hatahivyo tatizo linatokea baada ya kukutwa pikipiki nyingi zina madeni hivyo jamii kujikuta gharama ya kubadili inakuwa kubwa.

Hatahivyo amesema muda uliotolewa na mfupi lakini akasisitiza kuwa wameongea na wabunge wengine na kumshawishi waziri wa fedha ili atafute namna ya kuongeza muda jambo ambalo litapatiwa jibu hivi punde.
Ameongeza kuwa kumekuwa nchi kama Marekani rais akiondoka madarakani na watendaji wote wa serikali wananondoka, hivyo watendaji wa Tanzania wasiharibu kazi kwa kisingizio cha kuondoa vyama madarakani kwasababu wao watasalia, kuwa hiyo ni kuwatesa wananchi.

Mbunge huyo amesema suala la viwanja tayari limeanza kushughulikiwa na fidia zitarekebishwa kwa waliopimia, na hiyo imeanza mara moja tangu katibu m,wenezi CCM taifa alipoondoka Bukoba.
Na mwisho amesema CCM ni ile ile, wananchi walewale na mbunge ni Yule Yule, hivyo kugombea kuko palepale kwa lengo la maendeleo ya wananchi.



 


 

Na Mwanaharakati.

No comments: