MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 16 March 2015

SOMA HABARI KAMILI, ALIVYOPAMBANA NA MAMBA KWA NUSU SAA

MWENYEKITI wa Kamati ya Shule ya Msingi Udasi mwambao mwa Ziwa Tanganyika, kata ya Kabwe wilayani Nkasi mkoani Rukwa, Ismail Ndomboya (42) amenusurika kuuawa na mamba kwa kupambana kijasiri na mnyama huyo kwa zaidi ya nusu saa.
Hata hivyo, licha ya kuokoa maisha yake mnyama huyo katika mapambano hayo alimng’ata na kumnyofoa mkono wake wa kulia na kutokomea nao ziwani...............


Diwani wa Kata ya Kabwe, Asante Lugwisha akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya siku alithibitisha kutokea kwa mkasa huo uliotokea juzi saa moja na nusu jioni wakati Ismail alipokuwa akioga katika Ziwa Tanganyika kijijini Kabwe.

Akisimulia mkasa huo , Diwani Lugwisha alibainisha kuwa jioni hiyo ya tukio Ismail aliamua kwenda kuoga ziwani wakati huo akiwa pekee ndipo ghafla mamba alimvamia ghfla na kumuuma mkono wake wa kulia.

“Kwa ujasiri mkubwa Ismail alipambana kufa au kupona na mnyama huyo kwa nusu saa huku akipiga yowe akiomba msaada lakini hakuna aliyejitokeza kumsaidia kwa sababu sehemu aliyokuwa akioga ilikuwa mbali na makazi ya watu,“ alieleza.

Aliendelea kueleza kuwa hatimaye mamba aliunyofoa mkono wa kushoto wa Ismail na kutokomea nao ziwani ndipo Ismail alipokimbia kuelekea nyumbani kwake akiwa uchi.

“Baadaye nilitaarifiwa kuwa Ismail ameshambuliwa na mamba wakati akioga ndipo nilipofika nyumbani kwake, na tulijipanga tukamkimbiza katika Hospitali Teule ya Wilaya (DDH) mjini Namanyere ambao tulifika saa nne na nusu usiku ambako amelazwa kwa matibabu “ alieleza.

Mtaalamu wa afya wa Hospitali ya Wilaya, ambaye alikiri kuwa si msemaji, alikiri kupokelewa kwa mgonjwa huyo aliyejeruhiwa na mamba ambapo aliielezea hali yake kuwa inaendelea vizuri.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda amethibitisha kutokea kwa mkasa huo na kwamba uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

Na Mwanaharakati.

No comments: