Katibu mkuu kiongozi wa jamuhuri ya muungano wa tanzania Balozi Ombeni Sefue ametoa taarifa hiyo baada kukabidhiwa ripoti ya uchunguzi dhidi ya katibu mkuu huyo wa zamani Eliakim Maswi.
Uchunguzi uliofanywa kuhusu tuhuma za Maswi kuhusishwa na sakata la TEGETA ESCROW, imebainika kuwa Maswi
hana hatia na hajausika kwa namna yeyote kwenye kashifa hiyo.
Hatahivyo ripoti hii dhidi ya Mawsi tutaikabidhi kwa Mh
Rais kwa lengo kuwa aipitie tena maana yeye ndiye mwenye mamlaka ya uteuzi wake,
na ndiye aliyeniagiza nimsimamishe kwa uchunguzi mwishoni mwakajana, hivyo
ataangalia utaratibu mwingine.
Maswi aliyekuwa kitibu mkuu nishati na madini alisimamishwa na Balozi Sefue kuanzia
Jumanne, Desemba 23, 2014, kwa kutumia
madaraka aliyonayo kama Mamlaka ya Nidhamu kwa Watumishi wa Umma wanaoteuliwa
na Rais, wakiwemo Makatibu Wakuu.
Hatahivyo Balozi Sefue alimkaimisha ukatibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi C. Mwihava, hadi uchunguzi dhidi ya Ndugu Eliakim C. Maswi ulipotakiwa kukamilika.
Taarifa hiyo ya Balozi Sefue pia ilikariri kauli ya Rais Kikwete katika hotuba yake kwa Taifa jana, Jumatatu, Desemba 22, 2014 ambako Rais alisema yafuatayo:-
“Kuhusu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, kwa vile ni Mtumishi wa Umma, anatawaliwa na Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma, hivyo nimeshaelekeza Mamlaka kuchunguza tuhuma zake na hatimaye ikibainika ana makosa hatua za kinidhamu zitachukuliwa.”
Ndugu Maswi, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Ndugu Frederick Werema pamoja na Mawaziri wawili walituhumiwa wakati wa Kikao cha Bunge kilichopita kuhusiana na Akaunti ya Tegeta Escrow.
Na Mwanaharakati.
.jpg)
No comments:
Post a Comment