MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 31 May 2015

HOTUBA; WASIRA AKITANGAZA NIA KUWANIA URAIS KATIKA UKUMBI WA B.O.T JIJINI MWANZA LEO




HOTUBAYA MHESHIMIWA STEPHEN WASIRA KATIKA KUTANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAISWA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

  1. Nianze kwa kutoa shukrani kwenu wote mlioacha shughuli zenu ili kuja hapa kunisikiliza. Kuja kwenu hapa kwa wingi ni ishara ya imani mliyonayo kwangu, Nawashukuru sana
  2. Kwa zaidi ya mwaka mzima, kumekuwepo na miningo’no kuhusu uwezekano wangu kugombea urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Aidha kutokana na mijadala ya wananchi au kupitia mitandao ya kijamii au vyombo rasmi vya habari, mining’ono hiyo imefanya baadhi ya watu wanifuate ili wanishauri nigombee na wengine wamenipigia simu kwa kunishawishi nisisite kugombea
  3. Leo, nakuja hapa Mwanza kuvunja ukimya na kumaliza minong’ono kwa kutangaza rasmi kwamba nimekata shauri kugombea nafasi ya urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania


KWANINI NAGOMBEA

Zikosababu kadhaa, ambazo zimenisukuma kugombea kufikia uamuzi huo

  • Haki yangu ya kikatiba. Hii ni sababu ya msingi lakini siyo yenye uzito, kwa vile ni haki ya kikatiba na ni kwa ajili ya watanzania wote. Hivyo zinahitajika sababu za ziada licha ya haki ya kikatiba
  • Naifahamu Tanzania, Kwa muda mrefu tangu miaka ya 1970 nimeshirikishwa katika uongozi wa nchi yetu tangu nikiwa na umri wa miaka wa 27


  • 1970 kwa mara ya kwanza nilichaguliwa kuwa mbunge wa Mwibara katika wilaya ya Bunda
  • 1973 niliteuliwa kuwa waziri mdogo (Juniour Minister)
  • 1975 Niliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara na katibu wa TANU wa mkoa
  • 1982-1985 Afisa mwandamizi mkuu ubalozi wa Tanzania Marekani
  • 1987-1989 Raisi alniteua kuwa naibu waziri wa serikali za mitaa na mifugo na vyama vya ushirika
  • 1989-1990 Niliteuliwa kuwa Waziri wa kilimo, mifugo
  • 1990-1991 Mkuu wa mkoa wa pwani na katibu wa CCM Mkoa
  • 2005-2015 Waziri wa wizara ya maji , kilimo, ofisi ya Waziri mkuu Kilimo tena Ofisi ya rais mahusiano na uratibu na hatimae kilimo tena hadi sasa

Shughulihizi chini ya Marais wa awamu zote nne umenipa uzoefu mkubwa wamasuala ya kitaifa na kuniwezesha kuifahamu vema Nchi yetu. Mimi nimiongoni mwa Watanzania wachache, wanaoijua Tanzania ya leo nakubashiri Tanzania ya kesho.
Kamamwanafunzi mzuri wa nafasi mbalibali, walioniundisha waliozingatiahazina ya uzoefu, naamini uzoefu niliopata utanisaidia sana katikauongozi wa nchi yetu iwapo chama changu kitanipendekeza na hatimayekuchaguliwa na watanzania kwa Rais wa nchi yetu
Pamojana yote hayo haitakuwa rahisi kwangu kufanya uamuzi wa kugombeanafasi ya urais. Hii ni kwa sababu natambua majukumu na wajibu waRais ulivyo mzito wa kuongoza watanzania karibu million hamsini (50)na zaidi kwa ulinzi wa matumaini na matamanio yao ya nyakati.
Hatahivyo, baada ya tafakuzi nimeridhika kuwa uamuzi wa kugombea nafasihii ya juu kabisa katika nchi yetu ni sahihi na ni wakati mwafaka nahali ya kisiasa ilivyo kwa sasa, najiona kuwa mtu sahihi , kwa kuwaninayo nia ya kuipeleka nchi yetu katika ngazi ya juu zaidi kisiasa,kiuchumu na kijamii.
SERAYA JUMLA ZA NCHI
Baadaya maelekezo hayo ya utangulizi, sasa nizungumzie mambo ya msingi nahazina yanayohusu uongozi wa nchi yetu.
Endaponitateuliwa na chama changu na kupata ridhaa ya watanzania na hivyokuchaguliwa kuwa Rais wa Jamuhuri yaMuungano wa Tanzania nitaelekezanguvu zangu katika kusimamia yafuatayo;-

  1. Tanzania inabaki kuwa nchi imara yenye Umoja, Amani na Mshikamano.
  2. Taasisi nzito hususani mihimili mitatu ya dola ya kitaifa ( Serikali, Mahakama na Bunge) Zinaimaimarishwa na kuwezeshwa ili zitekeleze majukumu yake sahihi kwa mujibuwa katiba
  3. Utumishi wa umma utafanyiwa marekebisho ili utekeleze wajibu wake kwa uadlifu na waladi
  4. Kusimamia na kuhakikisha uchumi wa nchi unaendelea kukua kwa viwango vya juu zaidi ( kufikia tarakimu mbili) na utengenezaji wa nafasi za ajira unaoendana na matamanio ya wananchi
  5. Kuhakikisha raia wa Tanzania (wazawa) Wanawezeshwa ili washiriki kikamilifu katika kuendesha uchumi wa nchi yao.


CHANGAMOTOZINAZOIKABILI TANZANIA NA WATAZANZANIA
Haitoshikuifahamu Tanzania kama nchi na historia yake bila kuelewa changamotochangamoto zinazowakabili wananchi. Iwapo Chama change kitaniteuakupeperusha bendere ya CCM, na kupata ridhahaa, yako mambo manneambayo yatashughulikiwa na serikali ya awamu ya tano chini ya uongoziwangu. Mambo hayo ni;-

  1. Umasikini wa kipato

Pamoja na mafanikioya kukua kwa ..................uchumi na ungezeko la huduma za kijamii yaliyopatikanakatika awamu ya nne, bado ipo changamoto kubwa ya umasikini. Takwimuzilizopo zinaonyesha kuwa asilimia 28.2 ya watanzania ni masikini.Kwa mujibu wa takwimu hizo, wananchi wanaokabiliwa na umasikini huo,wengi wao wananishi vijijini na kujishughulisha na kilio, ufugaji nauvuvi. Uduni wa maisha ya vjijini unaotokana na hali hiyo yaumasikini ni chanzo pia cha umasikini wa mijini. Vijana wengiwanahama vijijini kwenda mijini na hivyo kuongeza kundi la umasikiniwa mijini.

LAZIMA TUWEKEZEKATIKA KILIMO

Njia pekee yakupambana na umasikini wa kipato hususani kwa wananchi wa vijijini ,ni lazima tuwekeze katika sekta ya kilimo, inayojumuisha kilimomazao, ufugaji na uvuvi. Serikali chini ya uongozi wangu, itatiliakipaumbele cha juu katika mapinduzi ya kiimo na uchumi wa vijijiniambao utaleta mabadiliko katia maisha ya watanzania walio wengi.

Kwa kuzingatiauwezekano mkubwa ambao Tanzania inao katika kilimo na idadi kubwa ya watu wanaoishi vijijini (70% - 75%) ambao wanaendesha maisha yaokutokana na kilimo na shughuli za kiuchumi wa vijijini, uendelezajiwake utapewa nafasi zaidi katika kuleta mabadiliko na kujenga uwezoambao baadae unaweza kuenezwa katika sekta nyingine. Mbinuzitakazotumika katika kuboresha kilimo ni pamoja na 


  1. Matumizi ya sayansi ya kilimo (kiimo cha kisasa na cha kibiashara)
  2. Utafiti wa huduma za ugani
  3. Kuboresha miundombinu ya vijijni hususani barabara, umeme, na umwagiliaji.
  4. Upatikanaji wa mikopo katika kilimo ili kubadilisha zana, hususan kuachana na jembe a mkono hatua kwa hatua hatimaye kuweka jembe la mkono katika makumbusho ya Taifa.
  5. Kuongeza thamani ya mazao ya kilimo kwa kuhusisha kilimo na viwanda.
  6. Kuwapatia wakulima masoko ya uhakika kwa mazao yao.


MIFUGO
Maendeleo ya mifugoyatazingatiwa ili kufanya tasnia hiyo iongeze uzalishaji na kuwabiashara ya kuaminika, kwa kuwekeza mipenyo ya matumizi ya ardhi ilikuhakikisha uzalishaji zaidi na ongezeko la thamani ili kuimarishamaisha ya wafugaji, Serikali yangu itaweka kipaumbele katikakusimamia matumizi ya ardhi hususan kutatua migogoro ya wafugaji nawakulima kwa ufupi yafuatayo yatatiliwa mkazo;-

  1. Kupima ardhi kwa nia ya kuwapatiawafugaji malisho ya mifugo yao.
  2. Kujenga malambo / mabwawa ili kuwapatia wafugaji maji hususani katika maeneo ya mifugo yao.
  3. Kuwapatia vikundi vya wafugaji mikopo kwa kutumia hati ardhi kama dhamana.


UVUVI
Uvuvi una uwezekanomkubwa wa kukua kwa kuzingatia Pwani kubwa, maziwa na mito ambayoTanzania imejaliwa. Serikali itaweka dhamira ya kuleta mabadilikokatika sekta hii ili iwe biashara yenye tija katika kuongezauzalishji zaidi na kuongeza kipato ch wavuvi.
Mkazo utakuwa zaidikatika kuimarisha vitendea kazi, kupanua masoko na kuhamasishauongezaji wa thamani kwa mazao ya uvuvi.

HATUA ZAKUCHUKUA.
Kwaujumla hatua zifuatazo zitachukuliwa;


  1. Kuhamasisha kilimo cha ufugaji na uvuvi wa kisasa na kibiashara kwa


  1. Kutumia maarifa ya kisayansi
  2. Zana za kisasa (kuweka jembe la mkono katika makumbusho)



  1. Mikopo na bajeti

Kuongeza uwekezajikwa njia ya


  1. Bajeti ya serikali ili kugharamia elimu ya wakulima, wafugaji na wavuvi
  2. Utafiti na uzalishaji wa mbegu za mifugo kilimo na mabwawa ya samaki
  3. Miundombinu ya umwagiliaji



  1. Mikopo

Mikopo toka benki yaKilimo Na Benki ya Raslimali


AJIRA KWAVIJANA NA MAENDELEO YA VIWANDA

Sualala ukosefu wa ajira kwa vijana ni kubwa kwa mujibu wa takwimu katikawizara ya kazi, vijana milioni moja wanaingia katika soko la ajiranchini kila mwaka kati ya hao ni vijana 200,000 tu ndio wanaopatakazi. Huu ni uwiano mbaya sana ambao kama hatushughulikiwa unawezakusababisha matatizo ya kijamii na kisiasa

Serikalinitakayoendesha itaweka dhamira ya kukabili changamoto hii ya ajirakwa kutazama zaidi ya ajira rasmi ili kujumuisha kujiajiri naongezeko la tija katika uzalishaji ili jujipatia kipato stahiki.

Katika kipindi chamiaka mitano ijayo, zitaendelezwa kitihada za kupata ufumbuzi wakupunguza tatizo la ajira nchini. Kipaumbele kitakuwa katika kukuzana kuanzisha viwanda vilivyo na uwezo wa kuajiri watu wengi kama vilevya nguo(Pamba), Korosho, Ujenzi na vyenye kuzalisha bidhaazanazotuwa na watu wengi wa ndani na nje.

Katika kipindi chamiaka mitano, serikali itahakikisha sekta za uzalishaji mali , kamavile kilimo, ufugaji, uvuvi , viwanda vikubwa vikubwa na vidogo nahuduma za kiuchumi kama mishati , uchukuzi na ujenzi vinatekelezamipango yao katika kupunguza umaskini na kuzaliza ajira 

Katika miaka yakaribuni vijana wameonyesha uwezo mkubwa wa kubuni ajira nakujiajiri, hatua ambazo zinastahili kupongeza kutiwa moyo na kuwezamfumo ya kuwawezesha. Ajira katika tasnia zilizokuwa kwa haraka nikatika masuala ya mitindo, miziki na filamu kama kina diamondplatinamz , Banana zoro na Binti yangu lady Jay dee, ommy Dimpoz,Christian Bella. Wabunifu wa mitindo kama vile Mustafa Hasani, AsiaIdarous, Filamu kama kina marehemu Stephen kanumba na Mtitu Gama.Leohii tasnia hizi zinaajiri mamlioni ya vijana.

Vijana mafundiwanatengeneza ajira katika Nyanja za ufundi, Viko viwanda visivyorasmi katika kila mji, kama uundaji bidhaa za vyuma, Ufundi bomba,Useremara, Ufundi umeme na umakenika wanatoa huduma kwa maelfu yawateja. Katika jiji la DSM mfamo gerezani na Tabata dampo na hapaMwanza makoroboi. Vijana wanajiajiri katika teknolojia mpya hasaTEHAMA. Wanaunda mifumo ya kusisimua ya kumpyuta na hata simu zamkononi na kumuwezesha mtumiaji kutatua matatizo mbalimbali.

Vijana na mifumo yausafiri wa umma kwa kutumia baiskeli, pikipiki na pikipiki za miguumitatu zimeongeza ajira.
Wafanyabiasharamaarufu kama wamachinga, hawa huuza chochote unachohitaji, kuanziamagazeti na mahitaji mengine. Kundi hili linahitaji kuwekewa mipangokwa kutengewa maeneo ya biashara badala ya kukamatwa kamata kilakukicha. Mama ntilie ni kundi linalotoa huduma muhimu ya chakula hasamijini.

Na Mwanaharakati.

No comments: