MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 26 May 2015

SIKILIZA KAULI YA MWISHO YA RWANGISA, TANGAZO LA KIFO CHAKE HAPA

Siku chache kabla ya kifo chake alizungumza nasi kwa njia ya simu kutokea New York Marekani, akisisitiza yafuatayo kwa wana Bukoba.

Baada ya kifo chake saa 5;00 asubuhi saa za huko, ambazo ni 12;00 jioni kwa afrika mashariki, baada ya kufanya mawasiliano na familia ya marehemu, mbunge Kagasheki alipewa taarifa kuwa taratibu za kusafirisha mwili zinafanyika tayari kuletwa Bukoba kwa maziko.
Bw. Samuel N. Luangisa ni nani?
Ni mzaliwa wa Bukoba mmoja kati ya waasisi wa TANU na hatimaye CCM, ambaye alipata kuwa mkuu wa mkoa wa kwanza wa baada ya uhuru (1961–1964), ambaye hatahivyo alikuwa miongoni mwa waliopendekeza mkoa huo kuitwa Kagera badala ya jina la awali la mkoa wa Ziwa magaharibi.
Jina hilo lilibadilishwa na kuwa “Kagera” mwaka 1979, mara baada ya vita kati ya Tanzania na Uganda, ambapo mkoa, chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa, aliyekuwepo wakati huo, Capt. Peter Kafanabo, ulipendekeza uitwe “Kagera”chini ya ushauriano wa mzee Luangisa.
 
SAMWEL RUANGISA alipata kuwa mbunge wa jamuhuri ya muungano kupitia jimbo la Bukoba mjini kwa tiketi ya CCM kati ya 1985-1990, na baada ya hapo ameendelea kuwa diwani wa kata Kitendaguro anakozaliwa hadi 2014 alipovuliwa udiwani na mahakama kutokana na mgogoro uliojitokeza na kushindwa kuudhulia baadhi ya vikao vya baraza la madiwani, akiwa miongoni mwa madiwani sita waliovuliwa kati ya madiwani 24 wa manispaa hiyo.  


Na Mwanaharakati.

No comments: