MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday, 14 May 2015

UZINDUZI BVR, WATALAAMU AMBAO NI VIONGOZI WAKISIASA WAMEKANA VYAMA VYAO KAGERA

. Wahapishwa kuthibitisha kujivua vyama vyao,
. NEC yasisitiza kusimamia sheria hiyo,
. Mgeni rasmiaeleza umuhimu wawapiga kura.

Uzinduzi wa semina hiyo umefanyika kwatika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kagera, na mgeni akiwa ni mkuu wawilaya Bukoba Jackson Msome, kwa niaba ya mkuu wa mkoa, kwa kuwasisitiza wanasiasa kutowaingiliawataalamuwakatiwa uandikishaji, na kusemakuwa ni dhaili kuwa wapiga kura ni muhimu lakini hawawezi kupatikana bila kuandikishwa, hivyo wahusika wahamasishe ipasavyo ili wajiandikishe wakutosha.
 
Viongozi hao kutoka ngazi ya halmashauri za mkoa wa Kagera za Bukoba, Muleba, Misenyi, Karagwe, Kyerwa, Biharamulo,na Ngara, wamehapishwa chini ya mwanasheria wa mahakama ya hakimu mkazi mkoani Kagera.


Afisa kutoka ofisi ya taifa ya uchaguzi NEC Bw ALBERT MACHA kutoka idara ya dafutari, amezungumzia kusimamia sheria zilizopitishwa,na hatua waliweka kuwa lazimazitekelezwe hasa kuhusu kujivua uanasiasa kwa muda.


Mwandikishaji maafisa uandikishaji wasaidizi na maofisa uchaguzi na waratibu wa uandikishaji wa mkoa wa Kagera, wameanza semina ya siku mbili mkoani humo, ili tarehe ya uandikishaji mkoani humo ikitangazwa  waweze kutimiza wajibu wao.


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), juzi imetoa ratiba ya kuanza uandikishaji kwa kutumia mfumo wa BVR katika mikoa ya Mbeya, Rukwa, Katavi  na Dodoma.
Kwa mujibu wa Tume hiyo, uandikishi litaanza siku ya ijumaa tarehe 15/05/2015 hadi siku ya jumapili kwa mikoa ya Mbeya, Katavi Rukwa na Dodoma. Uandikishaji utafanyika katika vituo vilvyoko katika vitongoji, mitaa na vijiji pamoja na kata zote za mikoa hiyo.

Aidha, vituo vitafunguliwa kuanzia saa 2.00 asubuhi na kufungwa saa 12 jioni, ambapo  Uboresshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura  utahusisha, wapiga wote upya ambao ni raia wa Tanzania kuanzia umri wa miaka 18, wenye kadi ya zamani watatakiwa kuirudisha  kituoni.

Mwananchi atachukuliwa alama ya vidole vyote kumi vya mikono  na kupigwa picha kisha atapewa kadi yake hapo hapo.

Na Mwanaharakati.

No comments: