MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 8 June 2015

HIVI NDIVYO POLISI ALIVYOKWIDWA, KIONGOZI CHADEMA KUTEKWA BAADA YA KUTAKA KUKIAMA CHAMA GEITA.




Jana wafuasi wa CHADEMA WILAYANI Geita mkoani humo, wamezuia gari la mfuasi ma aliyekuwa katibu wa chama hicho wilaya Bw Rogers Luhega, baada ya kutangaza kuacha nafasi ya uongozi na kutaka kujiunga na chama kingine, huku askari polisi aliyejulikana kwa jina mpoja la Zakayo wa kituo kikuu cha polis Wilaya ya Geita, akiokolewa baada ya kupigwa mara baada ya kuonekana akirekodi kwa kujificha kwenye mkutano wao uliofanyika katika viwanja vya soko kuu mjini Geita.
Sakata la kuzui gari la katibu huyo lilidumu kwa saa2, baada ya wafuasi hao zaidi ya 100 kusikia taarifa kuwa kada huyo wa CHADEMA aliyetangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Geita amekihama chama hicho na kwamba alitarajiwa kupokelewa na mjumbe wa NEC CCM Mkoa wa Geita  Leonard Bugomola.

“Tumesikitishwa kweli na taarifa hizi ndio maana tulizuia gari lake lisiondoke mpaka atueleze kama kweli amekihama chama, lakini ametuhakikishia yuko na sisi na tarifa hizo si za kweli, tungeshangaa sana manake juzi juzi hapa tumemchangia fedha za kuchukulia fomu leo hii atugeuke tusingekubali,”alisema Adriani Rwechungula na Ramudi Rasmusi.

Hata hivyo  Rogers  Luhega amekanusha madai ya  kuwa amekihama chama hicho na kujiunga na chama cha mapinduzi CCM mbele ya wafuasi hao, kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari na kuhusu kutimuliwa.

“Habari hii ya kujiunga na ccm na kwamba napokelewa na mjumbe wa nec ccm Mh. Leonard Bugomola si kweli jambo hili limeleta usumbufu sana watu wananizongazonga kila muda sasa niko mbele yenu nasema sijahama chama na wala sina mpango wa kuhama na kuhusu kutimuliwa mimi sijafukuzwa kama ilivyoripotiwa bali niliomba mwenyewe niachie nafasi hiyo ili nipate muda wa kutosha wa kupambana na ccm kuhakikisha tunalinyakua jimbo la Geita,”alisema Rogers Luhega.

Na Mwanaharakati.

No comments: