MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday, 7 June 2015

MAAMUZI YA KIKAO CHA NDANI CCM BUKOBA NA KINANA, WAHUSIKA KUTIMULIWA



. Nyaraka za uchunguzi mezani kwa mkuu wa mkoa, baadhi kufukuzwa maslahi ya wananchi,
. Kabla hajarudi Bukoba mwezi Agost RC atakuwa ameshamaliza kazi,
. Kinana apiga marufuku kutembelea nyumba za viongozi mara kwa mara,
. Wajumbe wakemea ujio wake kuwa vidonda badala ya neema.

Ni katika safari ya kuimarisha chama hicho mkoani Kagera, ambapo amekagua miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa katika manispaa ya Bukoba, na kuzungumzia mgogoro uliokuwapo katika chama hicho, huku akisisitiza wahusika kufukuzwa kwa maslahi ya wananchi na kuongeza kuwa watenda maovu wasijiite wana CCM.

Nyaraka mbalimbali kuhusu uchunguzi wa utekelezaji wa miradi ya upimaji viwanja, soko, na kituo cha kuoshea magari pamoja na stand ya mabasi, zimeshawasilishwa mezani kwa mkuu wa mkoa kutokana na uchunguzi wa CAG, hivyo maamuzi kwa wahusika yataolewa kabla ya tarehe 1 Agost kuhusu wahusika na ambao ni wananchama sikiliza kauli ya mkuu wa mkoa wa Kagea John Mongela hapa chini
Katibu mkuu wa CCM taifa Abdulrahman Kinana amesisitiza wana Bukoba kukumbuka mambo ya mvutano waliopitia, na kukubali kupokea maamuzi yatakayotolewa, kwani yatakuwa kwa maslahi ya wananchi wa Bukoba ambao leo wanataabika na hasa kwa kudhulumiwa, huku akisema kuwa ujenzi wa soko la gholofa kamwe siyo suluhisho la umaskini kwa wana Bukoba.
 
Ametolea mfano machinga complex ya Dar es salaam, kuwa wakati wowote itauzwa kulipa deni, ilhali haijawahi kuwanufaisha wafanyabiasha kwani wananchi wanatafuta bidhaa chini huku zikiozea juu ya jengo hilo kutokana na gharama zake na kutoonekana kirahisi kwao



Ni katika mkutano ambao umeudhuriwa na wananchi wa manispaa ya Bukoba waliokuwa na kiu cha kujua mstakabali wa ujenzi mradi wa soko ndipo Kinana akatoa kauli hii.
Katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Mayunga manispaa ya Bukoba, katibu mwenezi CCM taifa ndugu Nape Nnauye, amesisitiza kuwa kumejengeka desturi ya watu kutumia ofisi kufanya wizi, akisema kuwa hao ndiyo wachache wanaokichafua CCM , hukua kiongeza kuwa Balozi Kagasheki na mkakati wake kutetea wananchi wake kunafahamika, na anatosha kwa wakaazi wa Bukoba
Kabla ya mkutano huo, katika kikao cha ndani cha CCM, wajumbe wa kamati ya chama wilaya, wamevunja ukimya na kutaja mbinu mbalimbali zinazotengenezwa na mamluki, wanaotaka kukivuruga chama hicho, siyo kwa lengo la kuchukua nafasi tu, bali kuhakikisha wanaharibu ushindi wa chama hicho, kama wao hawatapata nafasi, huku wakimtaka KINANA kuacha amefukuza watu hao, ilhali mwenyewe akimwachia mkuu wa mkoa ili akirudi mwezi agost acute wameshaondolewa kwenye CCM.

Na Mwanaharakati.

No comments: