Mwenge wa Uhuru kuzindua miradi yenye thamani ya zaidi ya
shilingi bilioni 13 mkoani Kagera ambapo Mwenge huo ulipokelewa mkoani hapa
Wilayani Biharamulo Kata ya Kalenge
mpakani na Mkoa wa Kigoma tarehe 2/08/2015.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella akipokea Mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa
Kigoma Luteni Kanali Issa Machibya alisema kuwa Mwenge wa Uhuru utakimbizwa
mkoani Kagera katika Halmshauri zote za Wilaya saba na Manispaa ya Bukoba na
kupitia jumla ya miradi 52.
Katika miradi hiyo 52 Mwenge wa Uhuru utazindua miaradi 25,
utakagua miradi 12, utaweka mawe ya msingi katika miradi 13 aidha Mwenge huo
utapitia miradi mingine miwili ya kijamii ili kuhamasisha maendeleo kwa
wananchi wa mkoa wa Kagera.
Mhe. Mongella
alitaja mchanganuo wa gharama za miradi hiyo 52 itakayopitiwa na Mwenge wa
Uhuru kuwa serikali kuu imechangia kiasi cha shilingi 3,257,174,146 sawa asilimia 23.8 Halmashauri za Wilaya zimechangia kiasi cha shilingi 1,763,070,553 sawa na asilimia 12.9.
Aidha wananchi
wamechangia shilingi 3,086,502,508 sawa
na asilimia 22.5 wahisani wamechangia
shilingi 5,595,751,962 sawa na asilimia 40.8
ambapo jumla ya gharama yote katika Halmashauri za Wilaya na Manispaa ya
Bukoba katika mkoa wa Kagera ni shilingi 13,702,499,169 sawa na asilimia 100.
Mwenge wa
Uhuru wenye ujumbe usemao Tumia Haki
yako ya Kidemokrasia, Jiandiishe na kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa 2015,
Vijana wa leo na UKIMWI wazazi tuwajibike, Uteja wa Dawa za kulevya unazuilika
na kutibika chukua hatua, Wekeza kwa maisha ya baadae tokomeza Malaria, pia Kata
mnyororo wa Rushwa chagua kiongozi
mzalendo.
Ujumbe huo
unalenga kuwahamasisha wananchi hasa vijana kujikita katika shughuliza
uzalishaji badala ya kujihusisha na madawa ya kulevya, uteja, ngono zembe,
rushwa pia na kuchukua hatua dhidi ya
malaria pia wananchi kujitokeza kujiandikisha na kupiga kura wakati wa uchaguzi
mkuu 2015.
Mwenge wa
Uhuru uliopokelewa tarehe 2/08/2015 unatarajia kumaliza mbio zake mkoani Kagera
tarehe 9/08/2015 na kukabidhiwa mkoani Geita tarehe 10/08/2015 aidha
utahitimisha mbio zake kitaifa mkoani Dodoma tarehe 14/10/2015 na kukabidhiwa
kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete.
Na Afisa habari mkoa.
No comments:
Post a Comment