. Matukio 31
yachunguzwa na TAKUKURU,
. Upotoshaji wahusishwa,
. Wanahabari waaswa
kuwa makini.. Upotoshaji wahusishwa,
Akizungumza na mtandao huu juu ya malalamiko ya wananchi kwa kutaja RUSHWA kwa kila jambo mkoani Kagera, mkuu wa TAKUKURU Kagera RBC Joseph Mwaiswelo, amesema kuwa imekuwa ngumu kukomesha rushwa kama hakuna mlalamikaji kati ya mtoaji na mpokeaji.
Matukio 31 kuchunguzwa
TAKUKURU;-

Kuhusishwa upotoshaji;-
Katika kipindi cha kampeini hadi upigaji kura ya maoni kuelekea
kupata wagombea wa udiwani na ubunge katika majimbo yote ya mkoa wa Kagera,
TAKUKURU imepokea taarifa nyingi za uongo, hasa ambapo mtoa taarifa hasa kwa
njia ya simu anapotakiwa kuongozana na afisa na kushindwa kufanya hivyo.
Wanahabari waaswa
kuwa makini;-
Kutokana na baadhi ya maswali kwa wanahabari kuonekana
kuegemea sehemu au kwa mtu, afisa huyo wa TAKUKURU mkoa amewataka waandishi hao
kuwa makini, kutokubali kutumika na baadhi ya watu ili kuwachafua wenzao,
ilhali akisisitiza kuwa chombo cha habari kinatangaza au kuandika kupitia sera
ya chombo hicho na malengo ya mmiliki kama alivyoruhusiwa na mamlaka, hivyo
kuna haki zinazomlinda.
Katika mkutano huo, baadhi ya wanahabari wameonekana
kulazimisha kupata majibu ambayo hayawezekani kwa mujibu wa sheria na taratibu,
kwani hayaendani na baadhi ya maswali yaliyoulizwa wala hayahusiani na rushwa,
hivyo kuwataka kujua kanuni za taasisi husika kabla ya kuwatuhumu wahusika
wake.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment