Makundi mbalimbali yamejitokeza na kueleza mapendekezo yao ambapo miongoni mwa waliowakilisha ni mwenyekiti msaidizi wa machinga mkoa wa Dar es salaam , mwenyekiti wa shirikisho la watu wenye ulemavu Tz na mwenyekiti wa bodaboda.
Jaji
Joseph Sinde Warioba;
amewaeleza watanzania kuhusu sifa za wagombea wa CCM kuwa chama kimetazama sifa
tatu, uchapa kazi, uadilifu na uzalendo.
Amesema kuwa ukizungumzia uchapakazi wa
magufuli ni lazima uutazame katika vipindi vitatu alivyoudumu katika wizara
kadhaa hasa ya ujenzi ambayo imeiunganisha Dar es salaam na mikoa yote Tanzania
kwa barabara, akifanya kazi ndani na nje ya serikali.
Jaji huyo mstaafu, amesema kuwa alipewa
kazi na rais mkapa katika awamu ya tatu, ambapo alikuwa akichunguza rushwa na
kugundua ufisadi mkuu ulikuwa katika ujenzi ambapo katika kipindi cha miaka 20
tangu kuchunguza, Magufuli ameingia katika wizara hiyo kwa miaka 15 sasa na hakuna
tena taarifa za ufisadi katika ujenzi kama ilivyokuwa awali.
Chanzo kikuu cha ufisadi, amekitaja kuwa
ni kukaa karibu kwa viongozi na mafisadi, kwani taifa lina matatizo ya
kuporomoka kwa maadili ambapo kiongozi bora anatakiwa kuwa mzalendo bila kuwa
na makundi ila kundi moja ambalo ni watanzania.
Ameongeza kuwa mabadiliko yanayotajwa na
baadhi ya watu tayari yamefanywa na CCM kwa kiasi kikubwa kwa mara ya kwanza
baada ya kuweka wagombea wenye sifa hizo tatu na kubwa zaidi kumweka mwanamke
kama makamu wa Tanzania.
Rais
wa Zanzibar na mwakilishi wa baraza la mapinduzi; Dr.Ali Mohamed Shein
amesema kuwa ni wakati wa
watanzania kuenzi kazi kubwa iliyofanywa na Magufuli, na wazanzibar
wanayatambua, wakatuma salamu zao ili kudhiilisha ukweli wao, akisisitiza kuwa
uongozi siyo wa kujaribu hiyo watanzania wawe makini.
Rais
mstaafu wa awamu ya pili; Ali Assan Mwinyi amesema kuwa upinzani ni muhimu na
upo siku nyingi lakini siku imefika wao kuazima viongozi na dhamira ya
waliokwenda wameenda kuongeza nguvu ili kuishinda CCM lakini yawezekana ikawepo
CCM mbili A na B.
Rais wa awamu ya tatu; Benjamin Willaim
Mkapa, amesema katika hao nane walioteuliwa na tume ya uchaguzi, watanzania
watazame timu bora kwasababu ndiyo itasukuma maendeleo yao lakini watambue kuwa
hapa nchini kuna chama kimo tu cha ukombozi, huku akikumbusha sifa za viongozi
madhubuti kuwa ni wale wanaotekeleza imani za wananchi kwa vitendo, kushiriki
na wenzao, kuwa mstari wa mbele kutekeleza mambo ya umma kupitia ccm, wakati
wote mfano kauli zao na mtazamo wao kwa kutokuwa wazululaji.
Haitoshi kusema tu kuwa unachukia
umaskini bali masharti na taratibu za kuondoa umaskini.
No comments:
Post a Comment