MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday 29 August 2015

SLAA KUIBUKA UZINDUZI UKAWA JANGWANI LEO?

Picha ya maktaba.
Yapo mazungumzo ya chini kwa chini na sitofahamu kuhusu Wilbroad Slaa kuibuka katika mkutano wa uzinduzi wa kampeini za UKAWA kitaifa chini ya wenyeviti wenza, huku mgombea urais na mwenza wake wakitangaza ilani ya CHADEMA.

Itakumbukwa tangu Edward Lowasa kuingia CHADEMA baada ya kukatwa na CCM kugombea urais 2015, makatibu wa CHADEMA na CUF na ambao ni waasisi wakuu wa UKAWA, waliamua kukaa kando, huku Ibrahim Lipumba akitangaza adharani kuwa anaachia ngazi na kusalia mwananchama wa kawaida, ilhali Slaa hajawahi kujitokeza popote.

Maandalizi ya UKAWA leo yameshakamilika tayari kwa mkutano wao Jangwani jijini Dar es salaam.
Na Mwanaharakati.

No comments: