MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 30 August 2015

UPEPO WA SIASA WABADILIKA UKAWA NA CCM WAWA SUMU, MAZITO YAKO HAPA.



. Ni baada ya maneno mazito ya ACT,
. Yasema kazi ya rais inataka mtu imara,
. Chataja mambo matatu ya uchaguzi.

ACT- imefanya uzinduzi wake katika viwanja tofauti na CCM na UKAWA, baada kuzindulia viwanja vya ZAKHEM Mbagala, ambapo mshauri mkuu wa chama hicho Prof Kitila Mkumbo, ametumia dakika 10, kutaja kazi za rais, sifa na kuwasihi wananchi wapime na kuchagua October 25/2015.


Meneja wa kampeini za rais kupitia chama hicho Bw. Habib Mdunga, amesema kuwa watanzania wasidanganyike na vyama vya CCM na UKAWA, isipokuwa wakitaka ulaghai kuna vyama vitawalaghai, wakitaka mbwembwe kuna vyama vitawaonesha mbwembwe, lakini wakitaka sera waende ACT itawapa sera na utekelezaji wake.

Mgombea urais wa chama hicho ambaye ni mwanamke pekee kugombea urais katika vyama vyote Tanzania Bi. Anna Mgwila, ameeleza ilani ya ACT uku akisema mambo matatu ya utu, uzalendo na uadilifu na kuwa wamchague kuongoza taifa kwani mabadiliko yanayotakiwa kwa sifa ya kwanza ni mabadiliko ya kumpata kiongozi mwanamke Tanzania.


Na Mwanaharakati.

No comments: