MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 22 August 2015

WAGOMBEA UBUNGE WALIORUDISHA FORM MANISPAA YA BUKOBA


Ni Balozi Kagasheki ambaye amerudisha form hizo tayari kuanza kampein katika jimbo la Bukoba mjini, ambapo ahadi yake ni kueleza sera kupitia Ilani ya chama alichopitia cha CCM.
Mkurugenzi manispaa Aron Kagurumjuli kulia akipokea form za Mh Kagasheki.
Mwingine ni mgombea kupitia ACT Wazalendo, ambaye amesema kuwa chama chake kina mwongozo bora na tofauti na vyama vingine nchini hivyo wanajua jinsi ya kusogeza karibu maendeleo ya wananchi.

Mwingine ni kutoka TLP ambaye pia amesema wamejipanga vizuri kuchukua nafasi ya ubunge katika manispaa ya Bukoba ingawaje wanatambua kuwa hawana wananchama wengi Bukoba mjini.

Wilfred Muganyizi Lwakatare, yeye amerudisha form kupitia CHADEMA, akisema kuwa sasa ni wakati wake kurudia nafasi ya ubunge katika jimbo husika. 

Na Mwanaharakati.

No comments: