MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday 18 September 2015

MAKUBWA MKUTANO WA CCM KAHORORO SAUTI HIZI HAPA



. Waliohama vyama waulizwe wayasemayo wangeyasema?
. Watakiwa kumwogopa Mungu waseme ukweli,
. WanaCHADEMA waenda CCM.
Ni mkutano wa mgombea udiwani katika kata ya Kahororo manispaa ya Bukoba, ambapo makada na baadhi ya waliogombea kuwania ubunge katika kura za maoni, wamesema kuwa wananchi wasidanganywe na maneno yanayotengenezwa na waliohama chama, ili wao waonekane wazuri na wako sahihi, na kuwataka wananchi wawaulize wayasemayo wangekuwa CCM wangeyasema? Mzee Florence Mwakyoma, akasisitiza.
Katibu CCM mkoani Kagera Bw Idd Ame, amesisitiza sula la amani, kuwa vijana wasidanganywe kwa misingi ya viongozi kujitafutia nafasi, huku akisema kuwa mabadiliko yanafanywa na CCM kwa misingi ya chachu ya maendeleo wala siyo ombwe la uongozi kwani waliokuwa wanakwamisha chama chao tayari wameondoka.

Mwenyekiti wa bodi ya maji ambaye pia ni mgombea udiwani kata Kashai Samora
Lyakurwa amesema kuwa hundi ya malipo ya wananchi wanaodai fidia walishasainiwa na wahusika walijulishwa jinisi ya kupata fidia yao, hivyo wanaowadanganya hawana pa kufuatilia suala hilo kwani yeye ndiye muhusika mkuu.






Bwana Mjuni Kataraiya aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Bukoba mjini, ambaye pia alikuwa miongozi
mwa watia nia, amesema kuwa kura zao hazikutosha na hatimaye Kagasheki kupendwa zaidi kutokana na aliyoyafanya hivyo haoni aibu kumwombea kura kwani hakuna wakumshindanisha naye. 













Na Mwanaharakati.

No comments: