MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Sunday 25 October 2015

MATUKIO MAZITO NA PICHA YA UPIGAJI KURA BUKOBA





Wapiga kura katika manispaa ya Bukoba, wamejitokeza kwa wingi katika Vituo vya kupigia kura, kwa ajili ya kuwachagua Viongozi wanaowataka, kuanzia rais, mbunge na Madiwani,  licha ya dosari kadhaa zilizojitokeza.

Katika kata mbalimbali za manispaa ya Bukoba, wananchi wamejitokeza kwa wingi tangu Asubuhi na mapema na kujipanga katika mistari, kulingana na utaratibu ulioelekezwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini -NEC-.

Mgombea wa ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi CCM , jimbo la Bukoba mjini Balozi KHAMIS KAGASHEKI amepiga kura yake katika kituo cha National  Housing na kuelezea kuridhishwa kwake mwenendo wa upigaji kura.
 
Mkuu wa mkoa wa Kagera, JOHN MONGELA amepiga kura yake, katika Kituo cha Uwanja wa Ndege katika kata ya Miembeni na kuwahakikishia wananchi kwamba ulinzi kuwa umeimarishwa.

Amesema uandikishaji huoumeanza kwa wakati, ingawa kuna taarifa za baadhi ya vituo kuchelewa kufunguliwa kutokana na sababu mbalimbali.

Amesema kuwa katika baadhi ya vituo changamoto zilizopo ni za kawaida ikiwemo mawakala wa vyama kuchelewa pamoja na wasimamizi kuchelewa katika kupanga vifaa vya kupigia kura.

Bwana MONGELA ameonya kuwa mtu atakayejaribu kutaka kuvuruga amani katika kipindi hiki, Vyombo vya Ulinzi na Usalama, vitamchukulia hatua stahiki ili kuhakikisha Uchaguzi unakamilika salama.

Katika wilaya za Karagwe, Muleba na Missenyi, Bukoba Vijijini, taarifa zinasema kuwa upigaji wa kura unaendelea vizuri, licha ya baadhi ya Wasimamizi wa Vituo kuwa na kasi ndogo.

Taarifa hizo zinasema kuwa wananchi wamejitokeza kwa wingi kutekeleza haki yao ya kikatiba, licha ya baadhi ya watu hususan wazee kupata shida wakati wa kutafuta majina yao baada ya vituo kugawanywa.

Wapiga kura Elfu 71 na 600 katika manispaa ya Bukoba, wanatarajiwa  kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaendelea kote nchini, huku hali ya ulinzi na usalama ikiwa imeimarishwa kuhakikisha wananchi wenye sifa wa wanatekeleza haki yao kikatiba.

Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi  jimbo la Bukoba Mjini, ABDON  KAHWA   amesema kuwa Vituo  177  vinatumika  kupiga kura  katika  Kata  zote   14  za manispaa ya Bukoba.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: