MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 22 October 2015

BREAKING NEWS!!!VIONGOZI WA DINI HAWAKO TAYARI KUONA WANASIASA WANAUA WAUMINI BUKOBA



. Ni katika kikao maalumu cha ulinzi na usalama,
. Wasema na wao siasa wanaziweza ila wanafanya kazi ya Mungu,
. Baadhi ya wanasiasa CHADEMA kulazimisha wananchi kukaa mita 200.

Viongozi wa vyama vya siasa wametakiwa kuacha mara moja kuchochea wananchama wao kuleta vurugu wakati wa uchaguzi mkuu.

Hatahivyo wametakiwa kutambua kuwa  wanachama hao ndiyo waumini wa kanisa na misikiti, hivyo ghasia zitahatarisha siyo wanasiasa pekee kwani wanahitajika sehemu zote husika, dini na siasa.

Msaidizi wa askofu katika kanisa la Anglikan Canon Elisha Bililiza, amesema kuwa
viongozi wa dini nao wanaweza kufanya siasa, kufanya kazi ya ulinzi na sasa wanafanya kazi za kuhubiri waumini ambao hatahivyo ndiyo wanachama wa vyama vinavyoongozwa na wanasiasa, ambao baadhi yao wanawahamasisha wakae vituoni kulinda kura, jambo ambalo ni kinyume na sheria za nchi.



Hatahivyo makatibu wa vyama, akiwamo Sadick Amzakatibu  NCCR Mageuzi, Francis
Batu wa CUF na TLP, wamesema kuwa hawakotayari kuona wapiga kura wanasalia vituoni, kwani wanatambua utaratibu wan chi hauruhusu na hawataki kuwa chanzo cha kuondoa amani iliyodumu kwa miaka yote Tanzania.





Mkutano huo maalumu, umeitishwa na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo Bwana Jackson Msome, kwa kuwashirikisha viongozi wa dini, viongozi wa siasa na kamati nzima ya ulinzi na usalama pamoja na waandishi wa habari.

Na Mwanaharakati.

No comments: