MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 20 October 2015

MASIKITIKO; ULEMAVU WA UTATA MUHUSIKA AFICHWA NA KUTELEKEZWA



Shakira Abdallah mwenye umri wa miaka 24 ametelekezwa na mume wake kwa miaka minne baada ya kupata ulemavu wa viungo na hatimaye kushindwa kuongea.  

Mtandao huu umefanya mazungumzo na babu wa Shakira,  mzee Hamis Waziri anasema
kuwa katika kipindi chote cha uzima wa mjukuu wake alikuwa akiongea nae mara kwa mara kwa njia ya simu ili kujua hali yake na baadae mawasilainao ya kuongea yakashindikana, jambo lililowafanya washtuke walipoona ukimya ambao awali haukuwepo.



Sikiliza simulizi ya babu wa Shakira kama alivyozungumza na mtandao huu…


"Mama yake na bibi waliamua kuuza shamba na kufunga safari ili kumjulia hali mjukuu wao ambaye wakati huo alikuwa ameshalemaa na alikuwa hawezi tena kuongea.

Anasema kuwa mjukuu wake alichukuliwa kutoka Mtwara kwenda Dar na rafiki wa mama yake aliyekuwa akiishi jirani yao aliyejukana na kwa jina la Ashura kwa muda wa miezi sita hadi na kufanikiwa kupata mchumba aliyemuoa kwa ridhaa ya mjomba yake aishie.  

Waziri anasema kuwa kitendo cha mjukuu wake kupata ulemavu bila wao kujua ilikuwa ni pigo kubwa kwa familia  nzima kwakuwa mume wake alimteyekeza bila kumpatia huduma yoyote.  

“Mimba yake ilipofika miezi nane alikuwa akitupigia simu na kusema kuwa akiwa chumbani kwake anaona vitu vya ajabu ajabu hali ambayo ilitulazimu kumuomba mume wake amlete ili aweze kujifungulia huku lakini alikataa.

“Mjukuu wetu anateseka sana ukimuona huwezi amini kama alizaliwa akiwa mzima akawa anatembea na kuongea kitendo alichofanyiwa sio kitendo cha ubinadamu tunaomba serikali itusaidie ili aweze kupata stahiki zake kwakuwa hakupewa talaka na mume wake” alisema Waziri

 
Na Mwanaharakati.

No comments: