MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 2 October 2015

TAARIFA YA KUSIKITISHA KWA MNYONGE HUYU



Kufuata ugumu wa maisha unaoendelea kumkabili bibi  Zainabu Lipuga aliyekuwa akiishi juu ya dari na mjukuu kwa muda wa miaka mitatu sasa ameanza kuponda kokoto ili kujikimu huku. 

Mwandishi wa mtandao huu amemtembelea kuangalia maendeleo yake na kukuta bibi huyo, alisema kuwa ugumu wa maisha umepelekea apate shida kupata matibabu kwake na mjukuu wake.

Alisema kuwa kwasasa anajishughulisha na upondaji wa mawe ili kuuza kokoto ambazo zimekuwa zikimpa wakati mgumu kutokana na umri kuwa mkubwa hivyo kupata maumivu mara kwa mara.
 “Sio kwamba hizi kokoto ndio ambazo zinanisaidia hapana hizi zinaniongezea maumivu ya kifua na pia natumia nguvu nyingi kuponda wakati nauza kwa bei ndogo sana….

“Hali ya mjukuu wangu ndio inanifanya ni hangaike ili angalau apate chakula asilale njaa ila nasikitika sana ninanpoondoka kwenda kutafuta riziki lakini nikipata mfadhiri akamletea mjukuu wangu kiti nitafarijika sana kwakuwa atakuwa na uwezo wakukaa na mimi nje wakati naponda mawe kwakuwa ndio yanayotusaidia kuingiza kipato katika maisha yetu” alisema Lipuga


Na Mwanaharakati.

No comments: