Shirika la Umoja wa Mataifa la
Elimu,Sayansi na Utamaduni(UNESCO) limeendelea kuimarisha Redio za Jamii nchini
kwa kuwapa mafunzo ya mara kwa mara watendaji wa ngazi mbalimbali kwa lengo la
kuzifanya Redio hizo kuwahudumia vema wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini.
Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa
Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na
Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin
Yusuph amesema kumekuwa na mafanikio tangu mradi huo kuanza miaka mitatu
iliyopita chini ya ufadhili wa UNESCO, Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA) na
Serikali ya Uswizi ambapo licha ya kuwajengea uwezo vifaa vya kieletroniki
vilitolewa kwa Redio hizo.
Kongamano hilo la mwaka la siku tatu(3)
linafanyika katika Kituo cha Orkonerei Radio Service Simanjiro Manyara (ORS),
Terat wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara na limewaleta pamoja watendaji wa
Redio za Jamii 20 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Zanzibar .
“Tunalenga kuwajengea uwezo ili hizi Redio za Jamii
zifanye kazi kwa weredi ya kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi waweze
kushiriki mijadala inayohusu sekta za afya, elimu na kilimo,”amesema Yusuph.
Mshauri na Mkufunzi wa masuala ya vyombo vya habari jamii kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu akisistiza jambo katika mafunzo hayo. |
UNESCO inafanya kazi kwa karibu na Muungano wa Radio
za Kijamii Tanzania(COMNETA)unaongozwa na Mwenyekiti wake Sekiku Joseph.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment