MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 17 December 2015

KAULI NZITO YA MACK BOMANI KUHUSU SIAZA ZA ZANZIBAR



Jaji mkuu mstaafu Mac Bomani, amesema kuwa mbadala pekee katika uchaguzi wa Zanzibar ni kuondoa dosari zilizobainika, siyo kuishinikiza tume kutangaza matokeo yaleyale.
Akizungumza na waandishi wa habari katika kuonesha msimamo wake katika mambo kadha hapa nchini, jaj Bomani amesisitiza kuwa haiwezekani tume ya uchaguzi Zanzibar ikatangaza matokeo iliyoyafuta kwa sababu za kubainika makosa mbalimbali, kabla ya kuondoa dosari zilizobainika na kurudia uchaguzi, ili kuendelea kuaminika kwa wananchi.

Hatahivyo amesema kuwa mchakato wa katiba usiishie njiani kwani katiba inahitajika, hivyo baada ya uchaguzi wa Zanzibar ni muhimu lifuatiliwe kwani mengi yameshafanyiwa kazi kupitia waliohusika na mchakato huo hasa tume ya Warioba, kwani fedha nyingi imetumika na katiba mpya inahitajika.

Wakati huo jaj Bomani, amesema kuwa migogoro ya wakulima na wafugaji imekithiri nchini, jambo ambalo linasababishwa na kukosekana kwa mbadala kama ardhi ya kutosha hasa ya kufanyia malisho, na kuondoa taratibu za zamani zinazotumika kwa mfugaji mmoja kufuga ng’ombe elfu moja, ilhali hawezi kuwapa huduma ya kutosha, hivyo serikali iangalie katika sekta hiyo.

Ameitaja Tanzania kama nchi ya pili barani afrika kwa kuwa na ng’ombe milioni 42 ambao wanaweza kuinua uchumi wa nchi kwa kuingiza pesa za kigeni zingewekewa utaratibu kibiashara, kama ilivyo nchi ya Botswana  yenye wakaazi milioni mbili, mifugo michache ya ufugaji wa kisasa na kuuza tani laki 6 za nyama nchi za ulaya, tofauti na Tanzania inayoendekeza ufugaji wa kuhamahama na idadi kubwa ya mifugo na kuwa watumwa wa mifugo hiyo. 

Na Mwanaharakati.

No comments: