MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Thursday 17 December 2015

MAHAFALI YA CHUO KIKUU HURIA TANZANIA PINDA ASISITIZA-MSIKILIZE HAPA



Waziri mkuu mstaafu Mizengo Pinda, amesisitiza umuhimu wa elimu ya masafa ya chuo kikuu huria, kuwa ni muhimu kujiendeleza ukiwa mahala pa kazi.
Mh. Pinda amesema hayo wakati wa mahafali ya 29 ya chuo kikuu huria cha Tanzania, yaliyofanyika kwa mara ya tisa katika viwanja vya makao makuu ya chuo hicho Bungo Kibaha mkoani Pwani, kwa wahitimu 4,265 kutunukiwa shahada ya udhamivu, stashaada na ngazi ya cheti.

Amesema kuwa elimu ya masafa ilibezwa na kusababisha kiwango cha elimu nchini kutokupanda, akimwomba mkuu wa chuo hicho Dr Asha Rose Migiro, kudumisha mahusiano katika nchi za nje ili kupeana uzoefu jinsi ya ukuzaji wa elimu bora.

Udahiri wa wanafunzi wapya umeongezeka kutoka elfu 10 wa awali hadi laki moja  kwa muhula ambapo uongozi wa chuo hicho kwa sasa unafanya utaratibu wa kuendelea kutumia Tehama kufundishia ili kupunguza gharama za uendeshaji na kuweka majengo katika mikoa ambayo bado, na kufanya ukarabati katika baadhi ya maeneo.

Tangu chuo hicho kuanza hapa Tanzania, kimekwisha kuhitimisha wanafunzi 26,241, ambapo kimeweka vituo nchi za Rwanda, Namibia, Malawi na Kenya, na katika mahafali ya 29 mwaka huu, Bi Anne Kilango Malecela, mkuu wa mkoa Kagera John Mongela na aliyekuwa mkuu wa wilaya Kinondoni Jerry Slaa ni miongoni mwa wahitimu waliotunukiwa shaada.
 
Na Mwanaharakati.

No comments: