MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 4 January 2016

SERIKALI YAVUNJA UHUSIANO



Bahrain imetangaza kwamba imevunja uhusiao wa kibalozi na Iran, saa chache baada ya Saudi Arabia kuchukua hatua sawa.

Saudi Arabia iliwapa wanabalozi wa Iran siku mbili kuondoka nchini Saudi Arabia kufuatia mvutano uliotokana na kuuawa kwa mhubiri maarufu wa Kishia.

Bahrain hutawaliwa na Mfalme Msuni lakini raia wengi ni wa dhehebu la Shia.
Ufalme huo pia umewapa wanabalozi wa Iran saa 48 wawe wameondoka nchini humo.

Sudan nayo imemfukuza balozi wa Iran kutoka Khartoum huku muungano wa Jumuiya ya Milki za Kiarabu UAE nayo ikipunguza idadi ya maafisa wa ubalozi. Waislamu wengi nchini Sudan ni Wasuni.
Mhubiri huyo Sheikh Nimr al-Nimr aliuawa pamoja na watu wengine 46 baada ya kupatikana na makosa yanayohusiana na ugaidi.

Washia walishutumu hatua hiyo na maandamano yalishuhudia maeneo yenye Washia wengi.
Mjini Tehran, waandamanaji waliteketeza majengo ya ubalozi wa Saudi Arabia.

Saudi Arabia na Iran ndiyo mataifa makuu ya Kisuni na Kishia mtawalia Mashariki ya Kati, na yamekuwa yakiunga mkono pande pinzani katika mizozo inayoendelea Syria na Yemen.
Kuna wasiwasi huenda machafuko yakatokea kanda hiyo.

Jumatatu, misikiti miwili ya Wasuni ilishambuliwa na imam mmoja akauawa.
Saudi Arabia ilitangaza kwamba imekatiza uhusiano wake na Iran baada ya maandamano yaliyotokea ubalozi wake mjini Iran. Ilisema pia kwamba imemwagiza balozi wake arejee nyumbani.

Wizara ya mambo ya nje ya Iran imesema Saudi Arabia inaendeleza sera ya kuzidisha chuki na makambiliano katika kanda hiyo.

Msemaji wa wizara hiyo Hossein Jaber Ansari alisema Jumatatu kwamba Saudi Arabia inajaribu kusuluhisha matatizo yake ya kinyumbani kwa “kuyatoa nje kwa mataifa mengine”.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: