MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 4 January 2016

MAHAKAMA KUTOA HUKUMU BOMOABOMOA

Mbunge wa Kinondoni, Maulidi Mtulia akihojiwa na waandishi baada ya kutoka katika mahakama Kuu ya ardhi
Umati wa wananchi wa Mabondeni ikiwemo bonde la Msimbazi, Magomeni Mkwajuni, Hananasifu, Magomeni Sunna, Kigogo  na maeneo mengine wa Jimbo la Kinondoni wamefurika kwa wingi mapema kuanzia asubuhi ya leo katika Mahakama Kuu ya Ardhi iliyopo katikati ya jiji la Dar es Salaam kusikiliza kesi ya msingi ya kupinga kubomolewa nyumba zao iliyofunguliwa na Mbunge wa Jimbo hilo, Mh. Maulidi Mtulia (CUF).
 
Mtulia amefungua kesi hiyo kupinga kubomolewa kwa wakazi hao bila kuwa na njia mbadala ikiwemo kupatiwa makazi mengine kwa wananchi wake yenye usalama zaidi.

Hata hivyoi Modewjiblog iliyokuwa katika eneo la tukio tokea asubuhi, ilishuhudia umati mkubwa wa wananchi wakifurika katika viunga vya Mahakama hiyo kiasi cha kufanya shughulo zingine za mahakama hiyo kusimama.

Baada ya masaa matatu, Jaji wa Mahakama hiyo Kuu ya Ardhi, Mh. Panterine Kente aliweza kusimamia kesi hiyo huku baadhi ya wananchi wakiwakilishwa na wajumbe zaidi ya saba, pamoja na wanasheria wa Mbunge huyo, ambapo maamuzi yalidumu kwa muda wa saa zaidi ya saa moja,  na baadae Mawakili wa upande wa Mbunge wa Kinondoni, akiwemo Abubakari Salim aliweza kuutangazia wananchi hao pamoja na wanahabari kuwa, baada ya kupitia vielelezo vyote, kesi hiyo itatolewa hukumu kesho  siku ya Jumanne, Januari 5.2016.

“Kwa shahuri lililopo sasa linatarajiwa kutolewa jibu kesho  Januari 5, Saa tano asubuhi ndio tutapata jibu kamili, kwa sasa  tunarudi na tutakutana hapa hapa Mahakamani.” alieleza  Wakili huyo.

Na Mwanaharakati.

No comments: