MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 4 January 2016

UKUSANYAJI KODI WA IKABILI HALMASHAURI YA MANISPAA



Afisa uhusiano manispaa ya Ilala Bi. Tabu Shaibu, amesema kuwa katika mwaka  wa fedha 2010/11, walipanga kukusanya bilioni 2.8 lakini wakakusanya bilioni 2.1, mwaka 2012/13 walipanga kukusanya bilioni 4, lakini walikusanya bilioni 1.8, na hivyo kusababisha hasara serikalini, ambapo katika mwaka wa fedha 2015/16 manispaa inatarajiwa kukusanya bilioni 11.5.

Amesema kuwa viwango vya kodi ya majengo vimetajwa kweenye kifungu namba tatu, kifungu  kidogo cha kwanza cha sheria ya ardhi nyumba na makaazi, ambapo imefafanuliwa kuwa nyumba ya biashara na viwanda inatozwa 0.2% ya thamani ya jengo zima , nyumba  ya makazi inatozwa 0.15% kwa mwaka, huku akitaja sababu mbalimbali za kushindwa kutimiza malengo ya ukusanyaji kodi.

Meneja wa kodi ya majengo  halmashauri ya manispaa ya Ilala Bw. Kajuna, imejipanga kuanza utaratibu wa kuchukua taarifa upya kwa usahihi, kurahisha huduma za malipo kupitia mitandao ya kijamii, na kuanza kutuma ujumbe kwa kila mlipa kodi kupitia simu ya mkononi, ili kukumbushia deni na jinsi ya kulipa.

Novemba 2015, serikali ilitangaza kuanza kutumika kwa mfumo wa kielektroniki yaani ulipaji kwa njia ya mtandao  Tehama, kukusanya kodi za majengo na huduma mbalimbali, huku ikianzisha dawati la usaidizi kwenye halmashauri zenye shida ya mtandao, ili kuondoa ulipaji kodi kwa muhasibu, baada ya kubaini upotevu wa fedha zinazolipwa.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: