MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 4 January 2016

UBADHILIFU SERIKALINI SABABU YATAJWA


.Ni ukosefu wa mwongozo
Serikali kupitia wizara ya fedha, inaandaa mwongozo mpya chini ya sheria ya fedha namba 38, ili kuondoa ubadhilifu unaojitokeza nchini.
Mkaguzi mkuu wa ndani wa serikali Bw. Mohamed Mtonga, amesema kuwa sheria ya fedha inaelekeza kuandaliwa kwa mwongozo huo,ambao utahakikisha majukumu ya idara yanatekelezeka kwa kuwezesha wakaguzi wa ndani wanatimiza majukumu yao kwa kina, na kuhakikisha masuala ya utawala bora yanatekelezwa ipasavyo.

Hatahivyo bwana Mtonga amesema kuwa, idara ya ukaguzi wa ndani ina taarifa nyingi na nzito kuliko za CAG, ila zinahishia kwenye utawala kutokana na mfumo uliopo, kwa kusisitiza kuwa kuna uwezekano halmashauri  kupata hati safi baada ya utafiti wa ndani lakini ikawa tofauti baada ya kufanyiwa ukaguzi na  mkaguzi mkuu wa serikali CAG.


Idara ya mkaguzi mkuu wa ndani wa serikali, inafanyakazi katika wizara ya fedha ikiwa na vitengo vya uhakika wa ubora, usimamizi viashiria hatarishi, ukaguzi wa bajeti na mishaara, ukaguzi wa kiufundi na kitengo cha ukaguzi wa serikali za mitaa, ambavyo kwa pamoja vinanafasi ya kufanya ukaguzi maalumu wa kiuchunguzi, kulingana na mahitaji ya kitengo husika. 

Na Mwanaharakati.

No comments: