MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 24 May 2017

JINSI WAZIRI NA KATIBU WAKE WALIVYOFUTWA KAZI TANZANIA



Baada ya kukabidhiwa ripoti ya mchanga wa dhahabu, Rais wa Tanzania John Magufuli amemfuta kazi Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo.


Taarifa kutoka ikulu imesema uamuzi huo wa Rais umeanza kutekelezwa mara moja, na kuwa nafasi hiyo itajazwa baadaye.

Dkt Magufuli amechukua hatua hiyo saa chache baada ya kumshauri Prof Muhongo ajiuzulu.


Rais alitoa wito huo alipokuwa anapokea taarifa ya kamati maalum aliyoiunda kuchunguza mchanga wa madini uliokuwa katika makontena zaidi ya 200 aliyoyazuia yasisafirishwe, kwa ajili ya uchunguzi.

  • Rais Magufuli amfuta kazi katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini Tanzania

Ripoti iliyowasililishwa katika ikulu ya Tanzania, iliwasilishwa na kamati ya wataalam wa sekta ya madini kubaini aina na kiwango cha madini yaliyo ndani ya mchanga unaosafirishwa kwenda nje.


Katika makontena zaidi ya 200 yaliyokuwa yakichunguzwa, imebainika kuwa yalikuwa na dhahabu yenye thamani ya zaidi ya shilingi Trilioni moja za Tanzania.


Dkt Magufuli alivunja Bodi ya wakala wa ukaguzi wa madini Tanzania TMAA na kumsimamisha kazi Mkurugenzi wake kwa kushindwa kutimiza majukumu yake.


Na Mwanaharakati.

No comments: