Baada ya kukabidhiwa ripoti ya mchanga wa dhahabu, Rais wa Tanzania John Magufuli
amemfuta kazi Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo.
Taarifa kutoka ikulu imesema uamuzi
huo wa Rais umeanza kutekelezwa mara moja, na kuwa nafasi hiyo itajazwa
baadaye.
Dkt Magufuli amechukua hatua hiyo
saa chache baada ya kumshauri Prof Muhongo ajiuzulu.
Rais alitoa wito huo alipokuwa
anapokea taarifa ya kamati maalum aliyoiunda kuchunguza mchanga wa madini
uliokuwa katika makontena zaidi ya 200 aliyoyazuia yasisafirishwe, kwa ajili ya
uchunguzi.
- Rais Magufuli amfuta kazi katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini Tanzania
Ripoti iliyowasililishwa katika
ikulu ya Tanzania, iliwasilishwa na kamati ya wataalam wa sekta ya madini
kubaini aina na kiwango cha madini yaliyo ndani ya mchanga unaosafirishwa
kwenda nje.
Katika makontena zaidi ya 200
yaliyokuwa yakichunguzwa, imebainika kuwa yalikuwa na dhahabu yenye thamani ya
zaidi ya shilingi Trilioni moja za Tanzania.
Dkt Magufuli alivunja Bodi ya wakala
wa ukaguzi wa madini Tanzania TMAA na kumsimamisha kazi Mkurugenzi wake kwa
kushindwa kutimiza majukumu yake.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment