MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 10 May 2017

MWALIMU ALIYEFARIKI KATI YA 36 WA LUCKY VICENT AZIKWA KAGERA .









Mwili wa aliyekuwa mwalimu wa St. Lucky Vicent,Innocent Papian miaka 25 ambaye ni miongoni mwa watu 35 waliopata ajali may 6 huko Arusha na kupoteza maisha jana mwili wake umefikishwa wilayani kwao Kyerwa mkoani Kagera na kuzikwa.

Mkuu wa wilaya Karagwe Godfrey Mheruka akiwakilisha serikali ameongoza mamia ya wakazi wa mkoa wa Kagera na nje ya mkoa katika mazishi ya mwalimu huyo,huku akisema kuwa mwalimu Innocent enzi za uhai wake alikuwa anaiwakilisha vyema wilaya ya Kyerwa pamoja na Taifa kupitia taaluma yake ya uwalimu kwani alikuwa mtumishi ambaye hatiliwi shaka lolote kwenye vyeti vyake.
SAUTI YA MKUU WA WILAYA KARAGWE   

Kwa upande wake afisa elimu taaluma mkoa wa Kagera mwl,Fides Munyogwa amesema kuwa mkoa umepata pengo kubwa maana ni kijana ambaye ndo alikuwa ameingia kwenye taaluma lakini malengo yake yameishia njiani.

Pia Mwl,Munyogwa amewasihi wananchi kutoingiza imani yoyote juu ya kifo hicho kwani ni mapenzi ya Mungu badala yake wamuombee apumzike kwa amani.
"Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe".

MWISHO.

 

Na Mwanaharakati.

No comments: