Serikali
mkoani Kagera, imeanza kuchukua taadhari za ukaguzi wawageni wanaoingia nchini
kupitia mipaka ya mkoa huo, kujua kama wana maambukizi ya ugonjwa wa ebola
uliripotiwa nchini DRC.
Akizungumza
katika maadhimisho ya siku ya wauguzi kimkoa iliyofanyika katika hospitali
teule ya Rubya, mganga mkuu wa mkoa wa Kagera Dr. Thomas Rutachunzibwa, amesema kuwa ugonjwa huo haujaingia nchini
lakini wameanza kuchukua hatua za kuudhibiti.
Amesema
kuwa pamoja na ukaguzi kufanyika mipakani, tayari waganga wakuu wa wilaya
wameagizwa kuhakikisha wanatoa elimu juu ya ugonjwa huo kwa wananchi, ili
waweze kuutambua na kuchukua taadhari.
Akizungumza
na waandishi wa habari wiki hii, katibu wa wizara ya afya, maendeleo ya jamii,
jinsia wazee na watoto Dk. Mpoki Ulisubisya, aliwataka wananchi walioko katika
mikoa ya Mwanza, Kagera, Kigoma, Rukwa, Katavi na Songwe, kuzingatia maelekezo
yanayotolewa na wataalamu wa afya juu ya ugonjwa wa ebola.
Dr.
Rutachunzibwa amewataka wauguzi elfu
moja na 328 waliopo mkoani Kagera, kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na kiapo
cha kazi yao, ili kiwe mwongozo katika utendaji wa kazi zao.
Katibu
wa chama cha wauguzi mkoani Kagera –TANNA, Bi Georgina Sebastian, wakati
akisoma risala kwa mgeni Rasmi, amesema kuwa pamoja na mafanikio kwenye sekta ya afya mkoani humo, bado kuna
changamoto za ukosefu wa maeneo ya kutolea huduma kuwa na upungufu wa vitendea
kazi kama dawa na vifaa tiba.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment