MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Friday, 9 June 2017

MIPANGO WALIONAYO WASHIRIKI UMITASHUMITA MKOA WA KAGERA

MULEBA
 By Lameck Richard

Mashindano ya kupata washiriki wa Umitashumita Kitaifa yameendelea leo mkoani kagera huku watoto wa shule za msingi mkoani humo wakionyesha viwango vyao kwa lengo la kupata nafasi ya kushiriki mashindano hayo.

Kwa upande wake afisa michezo mkoa wa kagera Kefa Elias amesema kuwa mpaka sasa maandalizi ni mazuri na wanategemea kuanzia kesho wanaanza kambi rasmi itakayojumuisha washiriki 109 kutoka wilaya zote za mkoa Kagera mara baada ya mchujo kufanyika.
Aidha amesema kuwa timu hiyo itaendelea na kambi katika maeneo yaleyale ya chuo cha walimu Katoke kilichopo wilayani Muleba,ambapo watakaa hapo kwa siku saba na baada ya kambi watasafiri kuelekea jijini Mwanza katika chuo cha Walimu Butimba yatakapofanyikia mashindano ya kitaifa,huku akifafanua kuwa kikosi kitakachoenda kitakuwa na jumla ya wanafunzi  82,wanafunzi wenye mahitaji maalumu 15 na walimu 12,wote wa mkoa Kagera.
Akiongea kwa niaba ya Serikali afisa elimu taaluma mkoa wa Kagera Fides Mnyogwa amesema kuwa kufatia hali inayoonyeshwa na wanafunzi wa sekondari wanaoshiriki mashindano ya UMISETA jijini Mwanza,wanaamin hata hawa wa shule za msingi watafanya vizuri zaidi kuhakikisha mkoa wa Kagera unarudi na ushindi.
Mwl,Mnyogwa amewasihi wazazi na walezi kuendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa kuwaruhusu watoto wao kushiriki michezo kwani ni sehemu mojawapo ya ajira,huku akiongeza kuwa serikali inajitoa kuendesha mashindano hayo ili kuhakikisha wanaendeleza vipaji vya watoto mashuleni.

Picha za matukio mbalimbali katika mashindano hayo ngazi ya mkoa…………………………………………………


Na Mwanaharakati.

No comments: