MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 6 June 2017

WALICHOKISEMA WANAJIMBO LA MULEBA KUSINI KUHUSU HOTUBA ZA Prof.TIBAIJUKA BUNGENI



MULEBA

By Lameck Richard



 

Ikiwa vikao vya Bunge la bajeti vinaendelea mjini Dodoma,wabunge mbalimbali wamekuwa wakitoa hoja zao kwa wizara mbalimbali zinazojadiliwa ambapo na mbunge wa jimbo la Muleba Kusini Prof.Anna Tibaijuka amekuwa miongoni mwa watu wanaochangia.

Hivi karibuni ametumia dakika kumi kuchangia katika bajeti ya wizara ya Nishati na Madini ambapo katika hoja zake aligusia neno la “kadri unavyopanua ndivyo watu wanavyozidi kutamani”,kipande hicho kilianza kusambaa katika mitandao ya kijamii huku baadhi ya watu wakitumia neno hilo kwa malengo tofauti na anachodai alikuwa anaimanisha.

Kwa upande wake Prof,Tibaijuka amesema kuwa katika ulimwengu hawakosi watu wanaopenda kuingiza “propaganda”katika shughuli za maendeleo huku akisema kuwa yeye aliimanisha kupanua shughuli za maendeleo kama kupanua barabara,uwanja wa ndege,kupanua kilimo n.k ila watu wengine wanataka kutumia neno hilo kupotosha umma juu alichokuwa amelenga huku akiwasihi wananchi kuepukana na watu wa aina hiyo na badala yake wajikite katika mambo ya msingi kwa ajili ya maendeleo yao.

Wakiongea na vyombo vya habari kwa nyakati tofauti,baadhi ya wananchi wa jimbo lake la Muleba Kusini wamempongeza mbunge wao kwa uwakilishi anaouonyesha kipindi hiki katika kutetea masilahi ya wananchi wake hususani upande wa wafugaji na wakulima ikiwa ni pamoja na umeme chini ya mradi wa kusambaza umeme vijini “REA”ambao unatarajia kuanza kwa awamu ya tatu.

 Aidha wamesema kuwa bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya ubovu wa barabara katika baadhi ya maeneo na uhaba wa vituo vya afya hususani kata ya Biirabo ambapo wamemuomba kuweka nguvu zaidi katika sehemu hizo ili waweze kuepukana na changamoto hizo.

Sanjali na hayo,wameongeza kuwa kuna faida kubwa mbunge kutokuwa waziri maana awamu hii wameona jitihada alizonazo na anavyojitoa kuongea bungeni kwa kutetea jimbo lake tofauti na awamu iliyopita wakati akiwa mbunge na waziri na kumuomba asikatishwe tamaa na baadhi ya watu ambao wanabeza kile anachokifanya badala yake aangalie wananchi wamekwama wapi ili aonyeshe msaada wake.

TAZAMA WALICHOKIONGEA WANANCHI HAO KATIKA HII VIDEO……………………………………………..


Na Mwanaharakati.

No comments: