Shekh mkuu
mkoani Kagera Haruna Kichwabuta, amesema kuwa watachukua hatua kwa baadhi ya
waislamu waliotangaza kuwa waliofunga jumamosi wamefanya makosa.
Amesema hayo
katika ibaada ya Id el Fitri katika msikiti wa Jamiah mjini Bukoba, kuwa hakuna
anayemzuia muislamu mwenzake kuabudu
anachotaka, kwani wote ni watu wa mwenyezi Mungu na wanaruhusiwa kuabudu kwa
namna wanavyoamini.
Shekh Kichwabuta
amesema kuwa kilichofanyika jumamosi kwa baadhi ya waislamu kuzunguka na gari kutangaza na kuagiza waislamu kufungua siku ya
jumapili, kuwa hawana ruksa ya kufanya kilichofanyika kwasababu kila dini ina
msemaji wake na kama waislamu wafike hatua waseme sasa basi.
Amesema kuwa
huo ni utaratibu usiokubalika kwa kutumia uhuru vibaya kupitia mgongo wa dini,
na serikali inapochukua hatua wanalalamika kuwa wananyanyaswa na serikali yao,
na kwamba kuna misikiti mingi, hivyo kila muumini anaswalia anapoona panamfaha
kuliko kuvuruga wenzao.
Siku ya
jumamosi, Mufti mkuu wa Tanzania Aboubakar Zuebir alitangaza kuwa mwezi
haukuonekana, na kama kiongozi alifanya mawasiliano na wezake wa Zanzibar,
Kenya na maeneo mengine, na kumweleza kuwa mwezi haukuonekana na kutangaza Id
kufanyika siku ya jumatatu.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment