Mkuu wa upelelezi mkoa Kagera Max Kahindi amewataka wananchi kuwa wapole kufuatia matukio hayo
huku akiwataka kutoingiza chuki binafsi badala yake watoe ushirikiano kwa jeshi
la polisi ili kuhakikisha wanajua chanzo na mtu anayechoma nyumba hizo ili
hatua kali ziweze kuchukuliwa dhidi yake.
Aidha amewasihi wananchi kuhakikisha wanatoa taarifa za
kweli ili kumbaini anayefanya kitendo hicho huku akisema kuwa atakayebainika
ametoa taarifa za uongo kwa kumsingizia mtu ambaye hausiki naye pia atachukuliwa
hatua.
Pia ameongeza kuwa kitendo kinachofanyika ni kosa la
jinai,hivyo anayechoma nyumba hizo aache mara moja kabla hajachukuliwa hatua,na
amewaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa wale ambao wameguswa kwa kuwasaidia
huduma mbalimbali ikiwemo sehemu ya kuishi kwa muda wakati serikali ikiendelea
na upelelezi juu ya matukio hayo.
MWISHO.
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment