MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Wednesday, 21 June 2017

NYUMBA ZAIDI YA KUMI ZATEKETEA KIMIUJIZA WILAYANI MULEBA



MULEBA

 
Baadhi ya wananchi wa kata Mayondwe wilayani Muleba wamejawa na taharuka baada ya kuibuka hali ya kushangaza kufuatia nyumba zao kuteketea ghafla kwa moto mchana kweupe pasipo kujua chanzo cha moto huo.

Diwani wa kata Mayondwe iliyopo wilayani humo Method Bakuza amesema kuwa matukio ya nyumba kuteketea kwa moto wa ghafla yalianza may 4 mwaka huu katika kitongoji cha Ibila kijiji Bugasha ndani ya kata hiyo ambapo kufikia leo zimeteketea nyumba 12 ndani ya kitongoji hicho na haijulikani chanzo cha moto huo ni nini.

Aidha amesema kuwa moto huo unatokea muda wa mchana na unateketeza nyumba pamoja na migomba inayokuwa jirani huku akiongeza kuwa hakuna madhara yoyote yaliyotokea kwa binadamu labda mali zinazokuwa ndani ya nyumba zinaungua kabisa maana moto unakuwa mkali kiasi kwamba wanashindwa kuzima.

Kwa upande wake mmojawapo wa mashuhuda Jovenary Anatory amesema kuwa  nyumba ya kaka yake ni miongoni mwa nyumba zilizoungua na walikuwa ndani ya nyumba hiyo lakini moto umezuka ghafla na unaanzia kwenye paa na kuteketeza nyumba nzima.


MWISHO.                                                                                                             


Na Mwanaharakati.

No comments: