MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday, 20 June 2017

VIDEO;KESI ZAIDI YA 140 ZA MAUAJI ZIMEFUNGULIWA NDANI YA MWAKA MMOJA MKOANI KAGERA



BUKOBA                                                                                                                                                  


Kufuatia vitendo vya uhalifu vinavyoendelea katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania,mkoa wa Kagera umefanikiwa kufungua majalada ya mauaji zaidi ya 140 kwa mwaka 2016 kitendo kinachodhihirisha utendaji mzuri wa watumishi wa mahakama

Wakili wa serikali mkuu mfawidhi wa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali mkoa wa Kagera Hashimu Ngole amesema kuwa alipoingia mkoani Kagera mwaka 2015 alikuta kesi za tangu 2008 hazijafunguliwa majalada,kitendo kilichompelekea kuweka mikakati na mkuu wa upelelezi wa mkoa wa Kagera ili kuhakikisha kesi zinafanyiwa upelelezi na zinafunguliwa kwa uharaka.

Aidha amesema “mwaka jana 2016 ofisi yangu ilifanikiwa kufungua majalada ya mauaji kwenye mahakama kuu kufikia zaidi ya 140,na hii ni record katika nchi ambapo sio kitu rahisi kukipata”

Pia amezitaja changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni pamoja na malipo ya mashahidi wao kitendo kinachowakatisha tama baadhi ya mashahidi huku akisema kuwa kiutaratibu na kisheria wanaotakiwa kulipa gharama hizo ni mahakama.

MWISHO


Na Mwanaharakati.

No comments: