MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 19 June 2017

SERIKALI YATAKIWA KUCHUKUA HATUA ZA HARAKA KUOKOA MAISHA YA WAKAZI WA RWAMISHENYE

BUKOBA


Baadhi ya wakazi wa mtaa wa Kamizirente kata Rwamishenye manispaa ya Bukoba maisha yao yapo matatani kutokana ubovu wa miundombinu hususani eneo ilipofungwa Transfoma ya kusambaza umeme ndani ya mtaa huo. 

Barabara ya mtaa huo imeharibiwa na mvua,hali iliyosababisha kuwepo kwa shimo kubwa ambalo linmawapa wasiwasi wakazi wa maeneo hayo na watumiaji wa barabara hiyo kwani mtu akianguka ghafla ndani ya shimo hilo asilimia za kunusurika ni chache.

Kufuatia hali hiyo majirani wameiomba serikali kuchukua hatua za haraka kufukia shimo hilo ili kuweka maisha yao katika hali ya usalama,kwani  lipo eneo ambalo linatumiwa na watu wengi wakiwemo wanaofuata maji katika mto wa Kamizilente.


JIONEE PICHA MBALIMBALI ZA SHIMO HILO…………………………….......................



Na Mwanaharakati.

No comments: