MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Saturday, 17 June 2017

WANANCHI WATAHABIKA KUTOKANA NA UKOSEFU WA MAJI

MULEBA
 
Chanamoto ya uhaba wa maji imeendelea katika maeneo mbalimbali mkoani Kagera hali iliyosababishwa na baadhi ya vyanzo vya maji kukauka na kupelekea wananchi kutegemea chanzo kimoja.

Hali hiyo imewakuta pia baadhi ya wananchi wa wilaya Muleba kata ya Nshamba ambao wanahudumiwa na mto wa {Nyina Eshamba}ambao wamesema kuwa wanatumia  zaidi ya kilometa tano kufuata maji ikiwa ni sambamba na mto huo kuwa na watu wengi kitendo kinachopelekea kutumia muda mrefu katika maeneo hayo na shughuli nyingine kukwama.

Aidha wamesema kuwa wanakabiliwa  pia na changamoto ya uchakavu wa mabomba ya mto huo wanaoutegemea kitendo kinachosababisha wananchi kupata maji machafu.

Sanjali na hayo wameiomba serikali kupitia uongozi wao kuwasaidia juu ya changamoto hizo wanazokumbana nazo kwani ni sehemu mojawapo inayopelekea kukwama kwa kwa shughuli za maendeleo katika Taifa letu.




PICHA 4; SHUGHULI YA KUCHOTA MAJI IKIENDELEA {NYINA ESHAMBA}




Na Mwanaharakati.

No comments: