MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday, 12 June 2017

WITO ULIOTOLEWA KWA WATUMISHI WA SERIKALI NGAZI ZA MITAA

 BUKOBA

Watumishi katika ngazi za serikali za mitaa wametakiwa kuwa makini na kutunza vizuri kumbukumbu za mapokezi na matumizi ya fedha za umma zinazopelekwa na serikali kwenye vituo vyao vya kazi ambapo kuanzia julai mosi mwaka huu fedha zitapelekwa moja kwa moja kuliko ilivyokuwa zamani ambapo zilikuwa zinapitishwa katika halmashauri ndo zipelekwe vituo husika.


Wito huo umetolewa na mkurugenzi mtendaji wa manisapaa ya Bukoba Erasto Mfugale  katika ufunguzi wa mafunzo kwa maafisa elimu kata na wakuu wa vituo vya afya katika halmashauri za wilaya hiyo ambapo amesema mfumo huo utakuwa unafanana kwa nchi nzima na hivyo utasaidia kuondoa upotevu wa kumbukumbu za kiuhasibu zilizokuwepo hapo awali.

Aidha amewasihi watumishi hao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa umakini,na kutumia elimu watakayoipata ndani ya semina hiyo kwa wenzao na hatimaye watakuwa wamelisaidia taifa kusonga mbele kimaendeleo.



Na Mwanaharakati.

No comments: