Siku ya jana waisilamu walikuwa wanasheherekea sikukuu ya EID-EL-FITRI ambapo kwa mkoa Kagera manispaa ya Bukoba ilimalizika kwa majonzi baada ya watoto wawili mapacha kupoteza maisha pindi walipoenda kusheherekea na kuamua kuogelea katika beach ya Gymkana manispaa ya Bukoba.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Augustine Ollomi
amethibitisha kutokea kwa vifo hivo,na akiwataja waliopoteza maisha kuwa ni Hussein
Hamis na Hassan Hamis wakiwa na umri wa miaka 12 na walikuwa darasa la saba,watoto
wa askari kitengo cha usalama barabarani mkoani humo.
Aidha amesema kuwa walikufamaji majira ya saa kumi na moja
na dakika ishirini na tano jioni,na walizidiwa maji wakati wakiogelea kitendo
kilichopelekea wakitolewa wamekufa.
Sanjali na hayo Kamanda Ollomi amelaani kitendo cha
wanaochoma moto nyumba za wakazi wa wilaya Muleba,kijiji Ibila kata mayondwe
ambazo mpaka sasa hivi nyumba 13 tayari zimeteketea kwa moto na wananchi bado
wanadai hawajui chanzo cha moto huo.
TAZAMA VIDEO YA MKUU WA POLISI KAMANDA OLLOMI
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment