MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Tuesday 27 June 2017

HII NDIYO KAULI YA PROF. TIBAIJUKA KWA ALICHOKIKUTA JIMBONI KWAKE

 MULEBA


Mbunge wa jimbo la muleba Kusini lililopo mkoani Kagera Prof.Anna Tibaijuka ameungana na waisilamu na wananchi wa madhehebu mengine wilayani Muleba katika kusheherekea sikukuu ya EID akiwa mgeni rasmi katika baraza la EID wilayani humo. 

Kufuatia hafla hiyo iliyoandaliwa na Haji Shakiru Kyetema,imeibuka changamoto ambayo kupitia baraza la EID wilayani humo wamesema  kuwa kwa kipindi walichofunga wamegundua uwepo wa asilimia kubwa ya watoto yatima katika wilaya ya Muleba na hawapati msaada wowote kwa ajili ya kukidhi mahitaji yao,huku wakimuomba mbunge wao kutoa msaada juu ya changamoto hiyo.




Kwa upande wake Prof.Anna Tibaijuka amepokea changamoto hiyo na kumuagiza katibu wake kwa kushirikiana na uongozi wa wilaya kufanya sense ya kubaini watoto hao ili iwekwe mikakati bora ya kuhakikisha wanasaidiwa

Picha za matukio mbalimbali katika hafla hiyo 
 




Na Mwanaharakati.

No comments: