MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 24 July 2017

AUDIO; Mwananchi aliyeomba fedha za shule kwa rais afichua siri Kagera.



Bwana Pastory Kafundi ni mwananchi mkaazi wa kijiji cha Ngalalambi katika halmashauri ya wilaya Biharamaulo, ambaye alitumia nafasi yake kuomba rais awasaidie kuchangia ujenzi wa darasa katika shule ya msingi Mizani, baada ya wanafunzi kusomea chini ya mti tangu januari mwaka huu.

Akizungumza na macmedianews, mwananchi huyo amesema kuwa aliamua kujitoa muhanga kumweleza rais suala hilo, baada ya kuona kuna idadi kubwa ya wanafunzi wanaofikia elfu tatu katika shule hiyo ya msingi, na hata wengine kusomea chini ya mti ilhali wazazi na walezi wakiendelea kujitolea kujenga bila mafanikio kutokana na kukabiliwa na kero za miundombinu ya maji.


.
Mtandao huu umetembelea darasala hilo chini ya mti na kukuta mwalimu wake akiendelea kufundisha, kwa lengo la kujua kero anazokabiliana nazo katika ufundishaji wake huo.

Imebainika kuwa analazimika kutumia nguvu nyingi kuwashawishi watoto hao ambao mara nyingi wanapoteza muda kushangaa magari na wapita njia kutokana na mti huo kuwa karibu na barabara.


Wakati akipita katika kata ya Nyakaula, rais Magufuli alisimamishwa na kundi la wananchi wakitaka asikilize kero zao, ndipo mmoja wa wananchi aliyejieleza hapo juu, alipojitolea kumweleza rais hitaji lao juu ya ujenzi wa madarasa, na kumlazimu rais kutoa ahadi ya shilingi milioni 10 ambazo alizikabidhi kwa mkuu wa mkoa siku akihitimisha ziara yake Kagera kuelekea mkoani Kigoma.
Akikabidhi fedha hizo kwa uongozi wa shule na mbunge wa jimbo la Biharamulo, mkuu wa mkoa wa Kagera meja jenerali mstaafu Salum Kijuu, aliwataka viongozi na wananchi kuzitumia kwa malengo yaliyokusudiwa, nayeye kuwiwa kuchangia mifuko 10 saruji baada ya kuridhishwa na ujenzi unaoendelea shuleni hapo





Na Mwanaharakati.

No comments: