MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 24 July 2017

AUDIO; Mbunge ashambuliwa na wananchi wake Biharamulo, mjane azuiliwa kuonana na RC.

Wananchi katika halmashauri ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera, wamemlalamikia mbunge wa jimbo la Biharamulo, kutoonekana jimboni kwa kipindi kirefu mpaka rais alipofanya ziara.

Wakizungumza kwa jazba baada ya kumwona mbunge huyo kwenye mkutano wa rais Magufuli, wananchi hao wamesema kuwa wanazo kero nyingi ambazo kama angekuwa amezichukua kupitia nafasi yake ya mbunge zingeshafanyiwa kazi na serikali, hivyo hakuwa na sababu ya kuja wakati wa mkutano wa rais wala mkuu wa mkoa.
.
Katika maelezo yake kwa wananchi hao mbunge  Oscar Mkasa, amesema kuwa amekuwa akibanwa na shughuli za kibunge, ingawa mara nyingi amejitahidi kushughulikia baadhi ya kero za wananchi wake, akitaja mgogoro wa wafugaji wa Miongora kuwa aliutatua yeye, pamoja na kuomba shilingi milioni 200 za maji, katika mradi utakaotekelezwa na serikali.

Wakizungumza na mwandishi wa kituo hiki, wananchi wa kata ya Nyakaula katika halmashauri ya Biharamulo, wametaja kuwa wanakabiliwa na kero ya ukosefu wa huduma ya maji, uhaba wa vyumba vya madarasa mpaka kuwalazimu kutaja kero hiyo kwenye mkutanio wa rais, na baadhi yao kuchukuliwa maeneo kwa kufanyika uwekezaji wa visima vya maji bila fidia.
Bi. Mastula Hamis yeye ardhi yake ilitwaliwa na uongozi wa kijiji na kujengwa visima vya maji, lakini wakakiuka makubaliano ya kuwa analipwa kila mwisho wa mwezi na kuandikiwa barua kuwa atafidiwa eneo lingine ambalo hatahivyo hakuwahi kupewa, huku akizuiliwa kuwafikia viongozi wa ngazi ya juu mamlakani.

Akiwa ziarani mkoani Kagera, rais wa jamhuri ya muunagno wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli, aliwahidi wananchi kuwa atamtuma muhandisi wa maji, ili aweze kushughulikia huduma hiyo, kwani hilo ni jukumu la serikali, na kuchangia shilingi milioni 10 za ujenzi wa darsa katika shule msingi Mizani.
 

Na Mwanaharakati.

No comments: