MAC PRODUCTION STUDIO'S

MAC PRODUCTION STUDIO'S
KWA MATANGAZO YA BIASHARA REDIONI( 0767-814844)

Monday 24 July 2017

Mapacha walioungana wazaliwa tena nchini.

Watoto wawili walioungana kuanzaia kifuani mpaka tumboni wamezaliwa kwa njia ya upasuaji katika hospitali ya Misheni ya Bigwaa wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

Huku hali ya mama na watoto hao ikiendelea vyema na mapacha hao wakiwekwa kwenye chumba maalumu kwa uangalizi, ingawa wamezaliwa wakiwa wametimiza miezi 9 kama kawaida.

Baba mzazi wa watoto hao Luka Kimole amesema kuwa ni suala la kushangaza kupata watoto kama hao lakini kwakwe katu halichukulii kama mkosi bali neema ambayo imetoka kwa Mungu.

Kaimu Mganga mkuu wa hospitali ya Berega anasema kuwa hali hiyo kujitokezakatika  miaka ya sasa ni kutokana na malezi ya ujauzito.

"Mara nyingi akina mama wanapokuwa wajawazito hushauriwa kutumia baadhi ya huduma za tiba, kwa mfano Ferav na Folic ambazo zinawasaidia kwakiasi kikubwa kuzuia watoto kuzaliwa katika hali kama hizi lakini katika hili hatuwezi kuongea zaidi ni uchunguzi zaidi utafanyika kuona ni kwanini hali kama hzi hujitokeza kwa wingi hasa miaka ya hivi karibuni.

" Kwa nje waweza kuona kama watoto wawili ni vigumu kujua jeh kwa ndani ni miili ya wawili tofauti au kuna kitu kimoja kinawaunganisha, hivyo kuona kama inaweza kufanyika huduma ya kutengenisha.



Na Gsengo

No comments: