Wilaya ya Misenyi iliyopo mkoani Kagera imekabidhiwa rasmi
kituo cha afya Kabyaile kilichojengwa kisasa na jeshi la wananchi Tanzania JWTZ baada ya zahanati iliyokuwa maeneo
hayo kuharibiwa na tetemeko la ardhi lililotokea
mkoani Kagera September 10 mwaka jana.
Baada ya makabidhiano ya kituo hicho kilichokuwa kinajengwa
na jeshi la wananchi Tanzania,Waziri wa nchi,ofisi ya waziri mkuu
,sera,Bunge,ajira na watu wenye ulemavu JENISTA
MHAGAMA amesema kuwa jeshi limefanya kazi nzuri lakini ukarabati wa vitu
vidogovidogo vilivyobakia utafanywa na halmashauri kwa kushirikiana na mkoa
huku akisema kuwa fedha ya ukarabati wameshaitoa.
Waziri Mhagama amesema kuwa kwa mkurugenzi na watendaji wa
halmashauri ya wilaya Misenyi atakayetumia vibaya fedha hizo hawatamuonea
huruma badala yake watakula nae sahani moja kwani fedha hiyo imetolewa kwa
ajili ya kukamilisha miundombinu iliyobaki ili kituo hicho kiendelee kuwa
katika kiwango bora.
…………………………………..TAZAMA VIDEO YA WAZIRI MHAGAMA…………………………………
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa kata hiyo wameipongeza
serikali kwa hatua hiyo nzuri waliyofikia kwani wamewarahisishia huduma ya afya
kwa ukaribu tofauti na ilivyokuwa awali ikiwa ni pamoja na kuhaidi kutoa
ushirikiano wa karibu katika kulinda/kutunza kituo hicho.
PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI KATIKA UZINDUZI HUO………………
Na Mwanaharakati.
No comments:
Post a Comment